• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MTUMISHI MDOGO WA LEO, NDIO MKUBWA WA KESHO

Posted on: October 11th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS                                  

Viongozi waswaa kuacha kujikweza na kutumia  nyadhifa za uongozi walizo nazo vibaya na badala yake waheshimu kila mtumishi kwa nafasi yake. Kila mfanyakazi ni muhimu kwa nafasi aliyonayo ndio maana yupo kwenye utumishi wa umma. Watumishi lazima tujaliane  wenyewe kwa wenyewe na tuwe kitu kimoja.

Hayo yamesemwa na  Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokutana kusikiliza changamoto za watumishi wa tarafa ya Karatu uliowajumuisha walimu wakuu, walimu wa kawaida, watumishi wa afya, watumishi wa kilimo na mifugo, na maafisa watendaji kata na vijiji. Amesema lazima watumishi wawe na ushirikiano katika utendaji kazi, wakifanya hivyo watakuwa na mafanikio makubwa sana. Watumishi wanapaswa kupewa moyo na viongozi  na kutembelewa mara kwa mara katika mazingira wanayofanya kazi. Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa  unaofanywa na  watumishi katika ujenzi wa taifa letu.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na watumishi wa Tarafa ya Karatu

Mh. Kayanda amegusia kuhusu elimu amesema swala la chakula kwa wanafunzi lina umuhimu wa kipekee na limekuwa likitoa matokea chanya hasa katika shule ambazo wanafunzi wanapata chakula cha mchana. lakini pia kuna kuchangia walimu wa ziada wanaosaidia kufundisha watoto, Mh. Kayanda amesema ataendelea kuzungumza na wananchi ili waone umuhimu wa kuchangia hususani pale wazazi wanapokubaliana. Katika swala la utoro wa wanafunzi amesema watendaji wa kijiji na kata wanapaswa kusimamia na kudhibiti utoro wa wanafunzi, hata katika sheria ya elimu ya mwaka 1967 imeeleza bayana mamlaka za watendaji wa kijiji na kata moja ya jukumu lao ni kuhakikisha wanafunzi  watoro wanarejea shuleni.

Mh. Kayanda amesema swala la kunyanyua kiwango cha ufaulu ni jambo linategemea mafiga matatu. Amesema ufaulu unamhusu Mwalimu, ufaulu unamhusu Mwanafunzi na unamhusu mzazi au Mlezi. Amesema mmoja kati yao akikosekana hakuna muujiza unaweza kuongeza kiwango cha ufaulu. Mwalimu anaweza akajitahidi lakini mwanafunzi asijitahidi, mwanafunzi na mwalimu wanaweza wakajitahidi lakini mzazi asitoe ushirikiano. Lazima wote watatu wawe kitu kimoja ndipo waweze kuleta matokeo mazuri katika sekta ya elimu. Mh. Kayanda amesema kuna tabia imejengeka ya swala la walimu walewale kusimamia mitihani kila mwaka amesema swala hilo litafanyiwa kazi na kila mwalimu mwenye sifa ya kufundisha zaidi ya kipindi cha  miaka mitatu  na kuendelea kama inavyohitajika, atapewa nafasi ya kusimamia mitihani ya kidato cha pili na kidato cha nne.

watumishi wakimskiliza Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda

Mh . Kayanda amesema swala la kufanya mdahalo juu maendeleo ya hali ya taaluma ya wilaya ya Karatu litafanyika mwanzoni mwa mwaka ujao. Swala hilo litakusanya wadau wa elimu  na walimu wenyewe, amesema kuna mambo ambayo wadau wa elimu wanapaswa kusaidia na kuna mambo ambayo waalimu wanapaswa kuyafanya.

Naye Afisa elimu taaluma wa sekondari wa wilaya Mwl. Robert Sijaona akizungumzia uboreshaji wa ufaulu ili kupata wanafunzi wenye ubora zaidi, amesema serikali inafanya mabadiliko ya mfumo wa elimu hatua kwa hatua  kuendana na mahitaji. Amesema swala la kubadili mfumo wa haliwezi kufanyika ghafula. Mwl. Sijaona amesema kwa sasa serikali imeanza kuwapa semina za kujengea uwezo walimu wa KKK.  Ili kuongeza ujuzi wa kuwasaidia wanafunzi kujua kusoma   kuandika na kuhesabu. Amewapongeza walimu wa shule ya msingi kwa juhudi kubwa wanazofanya katika kujenga wasomi wa baadae. Ametoa raia kwa walimu  wa sekondari kufanya jitihada za hali na mali  kusaidia wanafunzi wanaoingia shule za sekondari kupata  hamasa za kufahamu masomo wanayo jifunza  kwa ufasaha. Amesema ipo changamoto ya kutumia lugha ambayo mwalimu akimsaidia mwanafunzi kwa karibu anaipokea vizuri. Amesema wanafunzi wanapishana uwezo wa uelewa kuna mwanafunzi anaelewa taratibu  na kuna mwanafunzi wanaelewa haraka. Wote hawa sisi tunapaswa kuhakikisha wanafikia matarajio ya ndoto zao.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa