• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WALIMU, MUWE CHACHU YA WANAFUNZI KUPENDA MASOMO

Posted on: February 21st, 2019



Afisa elimu sekondari amefanya ziara jana katika shule ya sekondari Baray na Shule ya sekondari Qang’dend. Katika ziara yake alipata wasaha wa kuwaasa wanafunzi  na kuzungumza na walimu lakini pia kuainisha mikakati yake ya kuinua kiwango cha taaluma.

Bi. Maina  amesema tunahitaji matokeo makubwa wekeni mikakati kuondoa division zero, na F kwenye masomo. Tutekeleze majukumu yetu vizuri na tuwapende hawa watoto, amesema kupitia mikakati yetu tuliojiwekea tuinue kiwamgo cha ufaulu. Amehimiza walimu kujaza fomu za opras, amesema kila mfanyakazi atapanda daraja kutokana na matokeo ya utendaji kazi. Walimu tunahitaji kufundisha vizuri na ili tupate matokeo tunahitaji msukumo kutoka ndani.

Tuna mikakati ishirini na tano tuliojiwekea kuinua kiwango cha ufaulu lakini walimu mnambinu zenu pia za kufundisha zitumieni. Jitoeni kufundisha vizuri, matokeo ya form four na form two hayaridhishi. Bi, Maina amesema atafanya ziara za kushitukiza mara kwa mara ili kuona kama mikakati yake inatekelezwa vizuri. Amechukua changamoto mbalimbali zilizoelezwa na walimu na ameahidi kuzifanyia kazi.

Bi, Dorothea Singano Afisa Elimu Msingi aliyeambatana na Afisa Elimu Sekondari amehimiza walimu kufundisha kwa kiingereza ili wanafunzi waweze kujibu vizuri mitihani yao. Amesema mwalimu lazima uwe na haiba nzuri, kwa sababu wanafunzi wanaiga vitu kutoka kwa walimu wao. Amesema lazima mwalimu uvae vizuri mavazi ya kiofisi, mwalimu ni mzazi na mwalimu ni mlezi ni vyema tuwalee watoto vizuri. Walimu tuna wajibu wa kuwasadia wanafunzi kutimiza malengo yao, na tunapaswa tuwaongoze na kuwashauri wanafunzi vizuri.

Bi Dorothea amewaomba walimu kuondoa migogoro kazini, na kuwe na utaratibu mzuri wa kushauriana kuhusu kazi. Lazima kuwe na lugha nzuri za mawasiliano kati ya mkuu wa shule na walimu lakini pia walimu na mkuu wao wa shule. Walimu tusaidiane kutatua migogoro yetu wenyewe ili isiende mbali, lazima tufanye kazi kwa umoja. Lazima tufundishe kwa ufanisi na ufanisi wetu utaonekana kwenye ufaulu wa wanafunzi.

 Bi Dorothea ameonya vitendo vya walimu kujihusisha na mapenzi na wanafunzi. Amesema mwalimu ni chachu ya mwanafunzi kupenda somo, tunawajibu wa kuwashauri wanafunzi. Tuwajenge wanafunzi ili watimize malengo yao na malengo yao yatatimia pindi watakapofanya vizuri kwenye mitihani yao.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa