• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WALIMU, MUWE CHACHU YA WANAFUNZI KUPENDA MASOMO

Posted on: February 21st, 2019



Afisa elimu sekondari amefanya ziara jana katika shule ya sekondari Baray na Shule ya sekondari Qang’dend. Katika ziara yake alipata wasaha wa kuwaasa wanafunzi  na kuzungumza na walimu lakini pia kuainisha mikakati yake ya kuinua kiwango cha taaluma.

Bi. Maina  amesema tunahitaji matokeo makubwa wekeni mikakati kuondoa division zero, na F kwenye masomo. Tutekeleze majukumu yetu vizuri na tuwapende hawa watoto, amesema kupitia mikakati yetu tuliojiwekea tuinue kiwamgo cha ufaulu. Amehimiza walimu kujaza fomu za opras, amesema kila mfanyakazi atapanda daraja kutokana na matokeo ya utendaji kazi. Walimu tunahitaji kufundisha vizuri na ili tupate matokeo tunahitaji msukumo kutoka ndani.

Tuna mikakati ishirini na tano tuliojiwekea kuinua kiwango cha ufaulu lakini walimu mnambinu zenu pia za kufundisha zitumieni. Jitoeni kufundisha vizuri, matokeo ya form four na form two hayaridhishi. Bi, Maina amesema atafanya ziara za kushitukiza mara kwa mara ili kuona kama mikakati yake inatekelezwa vizuri. Amechukua changamoto mbalimbali zilizoelezwa na walimu na ameahidi kuzifanyia kazi.

Bi, Dorothea Singano Afisa Elimu Msingi aliyeambatana na Afisa Elimu Sekondari amehimiza walimu kufundisha kwa kiingereza ili wanafunzi waweze kujibu vizuri mitihani yao. Amesema mwalimu lazima uwe na haiba nzuri, kwa sababu wanafunzi wanaiga vitu kutoka kwa walimu wao. Amesema lazima mwalimu uvae vizuri mavazi ya kiofisi, mwalimu ni mzazi na mwalimu ni mlezi ni vyema tuwalee watoto vizuri. Walimu tuna wajibu wa kuwasadia wanafunzi kutimiza malengo yao, na tunapaswa tuwaongoze na kuwashauri wanafunzi vizuri.

Bi Dorothea amewaomba walimu kuondoa migogoro kazini, na kuwe na utaratibu mzuri wa kushauriana kuhusu kazi. Lazima kuwe na lugha nzuri za mawasiliano kati ya mkuu wa shule na walimu lakini pia walimu na mkuu wao wa shule. Walimu tusaidiane kutatua migogoro yetu wenyewe ili isiende mbali, lazima tufanye kazi kwa umoja. Lazima tufundishe kwa ufanisi na ufanisi wetu utaonekana kwenye ufaulu wa wanafunzi.

 Bi Dorothea ameonya vitendo vya walimu kujihusisha na mapenzi na wanafunzi. Amesema mwalimu ni chachu ya mwanafunzi kupenda somo, tunawajibu wa kuwashauri wanafunzi. Tuwajenge wanafunzi ili watimize malengo yao na malengo yao yatatimia pindi watakapofanya vizuri kwenye mitihani yao.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa