• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA MAJI GANAKO

Posted on: June 12th, 2019

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Ndugu Mzee Mkongea Ally ametembelea mradi wa maji Ganako, kuona undelevu wake katika utoaji wa huduma ya maji. Mradi huu wa maji ulizinduliwa tarehe 07 Septemba 2017 na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Mwaka 2017 Ndugu Amour Hamad Amour.

Ndugu Mkongea ameridhishwa na mradi wa maji wa Ganako, amesema baadhi ya miradi imekuwa haidumu. Ndugu Mkongea amemuelekeza Mkuu wa wilaya kuchukua hatua kali za kisheria  kwa watu watakaojihusisha na kuharibu vyanzo vya maji na miundo mbinu yake.


Ndugu Mzee Mkongea akimtwisha mama plastiki ya maji alipotembelea mradi huo Ganako.

Mradi huu wa maji una kisima kirefu chenye uwezo wa kuzalisha maji lita 10,000 kwa saa, matenki 2 ya Lita 10,000 kila moja, Vituo 13 vya kuchotea maji (DPs), kati ya hivyo, 12 vipo Shuleni kwenye maeneo ya kusomea, bweni la Wanafunzi, Jikoni, nyumba za Walimu na 1 chenye midomo 3 kipo nje ya Shule kwa ajili ya Wananchi.

Mradi huu uligharimu jumla ya Shilingi 139,278,100/=, ambazo Wananchi walichangia Shilingi 5,000,000/=,Halmashauri shilingi 5,000,000 na mdau wa Maendeleo wa Shule yetu FOCTZ (Focus on Tanzania Community) kupitia Ndugu Richard Herriman alichangia Shilingi 129,278,100/=. 

Mradi wa maji unahudumia wanafunzi takribani 741, walimu 31 na wananchi takribani 234. Mradi umeendelea kusaidia wanafunzi na wananchi wa jirani kuwa na uhakika wa Maji shuleni kwa ajili ya matumizi mbalimbali.  Kupatikana kwa maji shuleni kumesaidia wanafunzi na walimu kupata muda wa kutosha wa kujisomea na kujifunza.  Mradi pia umewezesha shule kumwagilia bustani kwa ajili ya mbogamboga, hivyo kuimarisha afya za wanafunzi na kuiongezea shule mapato kupitia uuzaji wa mbogamboga hizo.  Huduma ya maji kupatikana hapa shuleni kumesaidia Wanafunzi kupata muda wa kutosha kujifunza.

 

Matangazo

  • Wasimamizi, Wasaidizi, na Makarani wa Vituo October 06, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

    September 23, 2025
  • WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

    September 23, 2025
  • WENYE SIFA WATAKIWA KUOMBA MIKOPO HALMASHAURI

    September 24, 2025
  • UKUSANYAJI WA MAPATO UNAZIDI KUONGEZEKA KARATU

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa