• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU WATEMBELEA MRADI WA MBUZI

Posted on: June 12th, 2019

Mradi wa Upendo katika kijiji cha Basodawish umetembelewa na kiongozi wa mbio za mwenge Ndugu Mzee Mkongea Alli. Mbio za mwenge wa uhuru umetoa cheti cha shukrani  kwa taasisi ya Food for his children ambayo inafadhili na kusimamia mradi huo.

Ndugu Mzee Mkongea amesema mradi huo wa mbuzi unatija sana, mbuzi wanaofungiwa  na kutunza kwa kupewa chakula inasaidia kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji. Amesema mbuzi na ngombe wanaoranda randa mtaani au wakati wa kuchunga wanaweza kuingia kwenye shamba la mtu. Ndugu Mkongea amesema kwa mfumo huo wa kufuga unaepusha mifugo kupatwa na magonjwa kama mbungo. Ndugu Mkongea ametoa tuzo ya shukrani kwa meneja wa mradi huo.

Awali meneja wa mradi huo Bi, Honorina Honorati amesema mradi huo ni moja kati ya miradi kumi. Amesema mradi huo umewawezesha wafugaji kujenga nyumba pia kupitia vikundi vyao wameweza kusomesha watoto wao na kujikopesha wao wenyewe. Bi, honorina amesema wamelenga kupunguza umasikini kwa kaya kupitia mradi wa mbuzi wa maziwa, mradi unampango mkubwa kwa miaka mitano ijayo kwa kuanzisha shamba lao kuzalisha mbuzi wenyewe.



Bi honoria honorati akipokea cheti cha alichokabidhiwa na mkimbiza mwenge kitaifa Ndugu Mzee mkongea 

 Taasisi hiyo imejikita katika kusaidia wananchi, wanafanya ufugaji bora na kupata uhakika wa chakula, afya bora na kuboresha kipato cha familia.Kikundi kilianza na wanachama 15 mwaka 2009 na kusajiliwa rasmi 06/03/2019 kikiwa na wanachama 47 na kupata namba ya usajili CSO.KRT/1842. Kikundi kilianza na jumla ya mbuzi 18 (mbuzi jike 15, madume 3). Hadi sasa kikundi kina jumla ya wanachama hai 47(wanawake 33 na wanaume 14), kimezalisha jumla ya mbuzi 292 (wapo mbuzi 172 na mbuzi 120 waliuzwa).

Kikundi cha UPENDO kimepiga hatua na kuongeza shughuli zingine za ujasiriamali kwa lengo la kuongeza pato la familia, kuweka na kukopeshana ambapo kina hisa za Shilingi 6,800,000.00  kwa kipindi cha miezi sita  na  ufugaji wa ng'ombe wa maziwa watatu (jike moja mwenye mimba, ndama mmoja na dume mmoja) wenye thamani ya Shilingi 2,500,000.00  

 

Mradi wa mbuzi umewezesha kuwa na manufaa kadhaa, Afya za familia zimeboreka kwa kutumia maziwa. Kuuza maziwa na kujipatia fedha za kuendeleza familia. Kuuza mbuzi na kujipatia fedha. Kuongeza mazao mashambani kwa kutumia mbolea ya mbuzi. Kupata elimu ya ufugaji wa mbuzi wa maziwa, kilimo bora, elimu ya afya, elimu ya ujasiriamali. Mradi umewawezesha wakinamama waweze kujitegemea na kupunguza utegemezi wanaume. Mradi umerejesha amani ndani ya familia.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa