• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

NAMNA YA KUEPUKA, ATHARI ZA SUMU KUVU

Posted on: January 31st, 2020

Sumu kuvu ni aina ya kemikali sumu inayozalisha ukungu au fangasi. Sumu kuvu inatokea kwenye mazao ya nafaka; mahindi, maharage, kunde na mbegu za mafuta. Shirika la afya duniani (WHO)katika taarifa yake limesema sumu kuvu huharibu karibu asilimia 25 au zaidi ya chakula kinachozalishwa duniani

Kuvu ni jina la kisayansi (Fungi) ambacho ni kiumbe hai, ambacho si mmea wala mnyama. Uanishaji wa kisayansi unavipanga katika himaya ya pekee ndani ya Eukaryota. Ekukryota ni kundi kubwa la viumbe hai ambavyo havina selli zenye kiini cha seli na utando wa seli. Wanyama, mimea, fungi wote tunaoona wanahesabiwa  humo hii ni kwa mujibu wa (wikipedia)

Kuvu (fungi) katika matunda yanayooza

Afisa Kilimo Bi, Twilumba Ngwale amesema nchini Tanzania ugonjwa huu ulikuja mwaka 2014 na kuibuka tena mwaka 2016 mkoani Dodoma. Anasema sumu haionekani kwa macho, wala haina harufu, haina rangi wala kionjo hivyo kuwa jambo gumu kujua kama ugonjwa umevamia nafaka. Ukungu unaotokana na sumu kuvu unaweza kuwa rangi ya kijani ya chungwa, kijivu njano au kutoa harufu ya uvundo.

Afisa kilimo Bi, Ngwale anasema mazao yaliyohifadhiwa kwenye ghala kama yataathirika kwa kuliwa na wadudu, Mazao yanauwezekano mkubwa wa kuathirika na sumu kuvu. Anasema sumu kuvu huathiri sana nafaka zilizoanza kuathiriwa na wadudu kwa sababu inakuwa rahisi zaidi kupenya kwenye nafaka. Bi, Ngwale anasema mazao ambayo hayajakauka vizuri ambayo bado yana unyevunyevu nayo yanakuwa katika athari kubwa ya kuathirika na sumu kuvu.

Bi. Ngwale anasema mahindi kama hayajavunwa shambani na wadudu wakabangua yanakuwa katika hatare kubwa ya kushambuliwa na sumu kuvu. Lakini pia kama mkulima atavuna mavuno ambayo hayajakauka vizuri shambani nayo yanakuwa katika hatare ya kuathririka na sumu kuvu. Bi Ngwale anasema watu wa (ITTA) the International Institute of Tropical Agriculture walichukua sample za udongo ili kufanya utafiti wilaya Karatu kuhusu sumu kuvu na majibu ya utafiti huo bado hayajaletwa. Anasema kwa sasa inashauriwa kutumia Alsafa ambayo ni dawa ya kibailojia inayotumika kudhibiti sumu kuvu kwenye mazao. Inatumika wakati Mahindi yanapoanza kuchanua mbelewele. Bi, Ngwale anasema karanga ni zao linaloathirirka sanaa kwa sababu ni rahisi sana kwa unyevu kuingia,  amesema hali ni hivyohivyo kwenye nafaka  kama mazao hayahifadhiwi  sehemu nzuri ni rahisi kuathirika. Bi, Ngwale anasema ni vyema wakulima wakahifadhi nafaka kwenye ghala linaloruhusu mzunguko wa hewa.

Bi, Ngwale anasema sumu kuvu inaweza kusababisha mtu kupata  saratani ya maini, kwa sababu kemikali hiyo inapingia mwilini inaathiri sana maini. Amesema kemikali za sumu kuvu zinasababisha pia upungufu wa kinga kwa  mwanadamu. Bi, Ngwale anasema sumu kuvu huathiri figo za binadamu na kuzorotesha ukuaji wa viumbe, binadamu na mifugo. Mazao yakiathirika na sumu kuvu inaathiri biashara ya mazao na matokeo yake ni soko la mazao  kufa .

Bi ,Ngwale anasema namna ya kuepuka madhara ya sumu kuvu lazima mkulima avune mazao yakiwa yamekomaa na kukauka vizuri. Mkulima anashauriwa kutenga Mahindi yaliyoathirika na fangasi kwennye mahindi ambayo hayajaathrirka na fangasi. Bi, Ngwale amesema Mkulima anashauriwa ahifadhi Mahindi Maeneo yasiyo na Unyevunyevu. Mkulima anashauriwa asianike mahindi kwenye udongo badala yake atumie turubai au kichanja  kuanika mahindi

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa