• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

NAPENDA KUWA MNAJIMU

Posted on: October 30th, 2018

Na Tegemeo Kastus

Matokeo ya kitaifa ya mtihani wa darasa la saba yaliyotangazwa hivi karibuni na katibu wa baraza la mitihani Dkt. Charles  Msonde yameiletea Halmashauri ya wilaya ya Karatu heshima  ya pekee kwa kutoa mwanafunzi aliyefaulu vizuri kwa kushika nafasi ya tatu kwa ngazi ya kitaifa. Mwanafunzi huyo Given Cosmas Malyango ndiye mwanafunzi anayeongoza kwa ufaulu vizuri kwa upande wa wanafunzi wa kike.

Given Cosmass Malyango ni mtoto pekee kwa baba na mama yake, ana umri wa miaka 13. Mama yake ni mwalimu wa shule ya msingi Sumawe Karatu na baba yake ni mwalimu shule msingi katika moja ya shule Mkoani Dar-es salaam. Alianza elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Dudiye mkoani Manyara ambayo ilikuwa shule ya serikali na alisoma kwa kipindi cha miezi sita mwaka 2010. Mama yake    Goodness Kirway alipopata uhamisho kwenda karatu, akafanya mtihani wa awali wa kujiunga na shule  binafsi ya  Tumaini Junior japo ufaulu wake haukuwa mzuri.

Given alipokuwa darasa la kwanza, katika shule ya Tumaini junior English medium school mtihani wa mwisho wa mwaka wa darasa la kwanza alishika nafasi ya pili kati ya wanafunzi arobaini. Darasa la pili katika matokeo yake akawa miongoni mwa wanafunzi wa tano waliofanya vizuri. Kuanzia  darasa la tatu mpaka la saba akawa mtu wa kwanza; licha ya uwezo wa darasani Given  ni kiongozi bora, amewahi kuwa dada mkuu msaidizi na baadae kuwa  dada mkuu, wadhifa ambao amemaliza nao Tumani Junior English medium school.

Given anasema yeye ni mtu anayependa kutunza mda, alipokuwa  shule alikuwa  anatumia mda vizuri anafanya kazi mda wa kazi na mda wa kusoma anautumia vizuri kusoma. Given anasema ya shule iliwapangia mda mzuri wa kusali kwa pamoja jioni na asubuhi. Lakini siri ya mafanikio yake ni kusali na kusoma kwa bidii, huwa anasali pia peke yake kabla kulala na wakati wa kuamka licha ya kusali na wenzake. Shule iliwapa mazoezi ya mtihani ya wiki na mitihani ya mwezi ambayo walikuwa wanashindana na shule nyingine kimikoa. Lakini pia anawanafunzi ambao ni marafiki zake alioshirikiana nao kimasomo na kwenye changamoto mbalimbali ambao ni Caster Sizza ambaye ni mwenyeji wa Musoma na Emmaculate Alex ambaye ni mwenyeji wa Moshi.

Tabia ya kusali amefundishwa na mama yake mzazi Bi, Goodness Kirway, Given anasema mama yake ni mfariji wake mkubwa na amekuwa akimpa moyo pindi anapopata changamoto katika maisha yake ya shule. Given anasema baba yake Cosmass Malyango pia ni mtu anayependa maendeleo, kupitia kusoma. Mzee Cosmass Malyango hapendi familia yake ipate shida. Given anakumbuka alishawahi kupoteza kiasi cha shilling 30,000 akiwa kwenye ziara ya kutembelea Hifadhi ya ziwa Manyara akafadhaika sana, lakini alipoomba mwalimu awasiliane na mama yake alipewa kiasi hicho cha fedha alichopoteza.

Changamoto alizozipata akiwa shuleni ni swala la kuamka asubuhi na mapema ili kujiandaa na vipindi vya masomo. Kadhia nyingine aliyokuwa akikabiliana nayo ni jinsi ya kuhamisha jibu kupeleka katika karatasi ya maswali. Given anasema kuna wakati alikuwa anakosea  majibu siyo kwa kutofahamu swali  bali ni ile hali kujichanganya wakati wa kuandika majibu.Given anasema yote tisa kumi ni swala la kushindwa na mwanafunzi wa Costigan kwenye mtihani wa PESNO uliofanyika mwezi wa tatu mwaka huu na kuzidiwa kwa alama mbili. Anasema ni bora hata angezidiwa kwa alama tano kumi siyo mbaya kuliko kuzidiwa kwa alama mbili.

Given anasema kuwa mwanafunzi wa tatu kitaifa haikutokea kwa bahati mbaya, alijipanga vyema katika masomo yake. Amesema jitihada hizi hazitaishia hapo anajipanga kwa miaka minne ijayo aweze kufanya  vizuri zaidi. Given anasema yeye anapenda masomo ya sayansi ingawa masomo yote anafaulu kwa uwiano sawa. Lengo lake ni kuja kuwa Mnajimu kwa sababu watu wengi wanaiogopa taaluma hiyo kwa sababu ya gharama za kusoma. Lakini wanaogopa kwa sababu wanaona kwenda angani kufanya utafiti wa kisayansi ni kwenda kinyume na mipango ya mungu. Given anasema mtu anayemhamasisha ni Mnajimu mwenye asili ya marekani anayeitwa Neil Armstrong. Given anasema atafurahi sana kama atatimiza ndoto zake hizo. Given anapenda kusoma Chuo kikuu cha Dar es salamu; madhari yake alivyoona kwenye picha ni mazuri, lakini kwa namna ambavyo Dkt Chris Mauki Mhadhiri wa chuo hicho alivyoelezea kuhusu chuo hicho, alipowatembelea wanafunzi hao shuleni kwao Tumaini Junior Karatu

Given pia anapenda michezo anacheza mpira wa pete nafasi ya kiungo wa katikati na anacheza mpira huo kama kiungo mshambuliaji upande wa pembeni. Given anasema anaweza kucheza mpira wa miguu wa wanawake, yeye hucheza kama beki wa katikati. Given anasema yeye ni shabiki wa klabu ya Barcelona na Yanga kwa Tanzania. Anapenda unyumbulifu wa Lionel Messi katika mpira wa miguu na  jinsi anavyotoa ushirikiano kwa wachezaji wenzake. Given amesema licha ya kupenda michezo yeye atajikita zaidi kwenye maswala ya taaluma.

Given anasema yeye akiwa nyumbani anapenda kumsaidia mama yake shughuli za nyumbani kupika kufanya usafi na mda wa ziada hutumia kuangalia katuni. Anaamini siku moja naye atakuwa jasiri, mama yake humuambia ukitaka maisha yawe magumu yatakuwa magumu na ukitaka maisha yawe rahisi yanakuwa rahisi. Pamoja na mafanikio ya Given, msingi mkubwa umebakia katika imani yake ya kusali  na kufanya kazi kwa bidii. Given anawahusia wadogo zake aliowaacha  shule ya msingi, ili wafanikiwe hawana budi wafanye kazi kwa bidii.

Bi, Goodness Kirway mama mzazi wa Given nasema mwane amempa heshima kubwa, anamini msingi mkubwa wa mafanikio upo katika elimu. Anakumbuka kitu kilichompa changamoto, ni wakati Given anaanza shule hakuwa na ufaulu mzuri kama mzazi akawa anamuombea ili afaulu vizuri na mungu anamemsaidia matokeo yanaonekana. Bi, Goodness, anasema anapenda mwanae awe Daktari wa binadamu, kwa sababu tangu alipokuwa mdogo alionesha nia ya kuwa daktari kwa michezo ile ya kitoto aliyokuwa anacheza nyumbani. Anakumbuka mwanae aliopokuwa mdogo alishamuambia babu yake anataka kuwa daktari ili afanye utafiti kwanini mtu akizeeka nywele zake zinabadilika nakuwa nyeupe. Bi, Goodness amesema licha ya kuwa anapenda mwanae kuwa Daktari anamruhusu kuendelea na ndoto zake kuwa Mnajimu.

Mwalimu mkuu Bi, Grace Benedict Saguma anasema, Given amempa amani sana, na amemjengea jina.  Bi, Grace anasema Given ananidhamu ya hali ya juu sana na alikuwa anasoma kwa bidii hayo yaliyotokea waliyatarajia .Bi, Grace anasema Tumaini Junior ni shule inayofanya vizuri sana  Wilaya ya Karatu kwa sababu ya mshikamano wao na hili lilitokea limezidi kuwatangaza zaidi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa