• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

NI VYEMA WANANCHI KUTUNZA VYANZO VYA MAJI

Posted on: December 8th, 2018


Na Tegemeo Kastus

Kikao kazi cha bonde la kati kimefanyika jana katika ukumbi wa Halmashauri, kikao hicho kililenga kuwajengea uwezo watendaji wa Halmashauri pamoja na kamati ya ulinzi na usalama juu ya sheria za usimamizi wa maji. Mkuu wa Wilaya ya Karatu Mheshimiwa Theresia Mahongo  alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho.

Katika hotuba yake ya ufunguzi Mheshimiwa Theresia amesema maji ni muhimu katika maisha ya binadamu na ndio maana tunasema maji ni uhai, katika maisha yetu maji yakikosekana hayana mbadala. Maji hutumika katika matumizi ya manyumbani, na yanatumika katika matumizi ya viwanda. Mheshimiwa Theresia amesema bila maji  hakuna samaki, mradi mkubwa wa Stigler  George unategemea maji na ni mradi utakaokuwa na gharama nafuu, uchimbaji wa madini unategemea maji na hata shughuli za usafiri majini zina gharama nafuu.

Mheshimiwa Theresia amesema  robo tatu ya mwili wa binadamu  ni maji, amesema kiasi cha maji kilichopo chini ya ardhi kimepungua na hii imetokana na uharibifu wa mazingira, ongezeko la shughuli za mifugo ambao wanatumia maji, ongezeko la watu na kuchoma misitu. Mifugo imesababisha vyanzo vya maji kufukiwa kutokana na mmonyoko mkubwa wa udongo. Ongezeko la watu imekuwa changamoto katika matumizi ya maji kutosheleza mahitaji. Amewaomba watendaji kusimamia na kutunza vyanzo vya maji, amesema sisi tunatunza chanzo cha maji cha ngorongoro ambayo sisi ndio tunatumia.

Mheshimiwa Theresia amesema kukosekana kwa maji kwenye hifadhi ndio kunasababisha wanyama kutoka kwenye hifadhi na kuja kwenye makazi ya watu kutafuta maji. Amesema sera ya maji (2002) inataka usimamizi shirikishi kupitia jumuiya  za watumia maji, ili kuepukana na migogoro ya maji. Amesema kuna kijiji kama Matala kuna visima 8 vya maji ambavyo  havitoi maji amemuelekeza Injinia wa maji wa wilaya kushughulikia swala hilo. Tufanye kazi ya kuelimisha wananchi kuelewa sheria za usimamizi rasilimali maji na kuzuiya uchafuzi wa maji hasa ukizingatia nchi inaenda kwenye uchumi wa kati ikiwa ni pamoja na kuzuia uchimbaji wa visima usioratibiwa.

Mheshimiwa Theresia ameomba wizara maji kutenga fedha kwa ajili kumalizia kuweka mipaka ya kudumu kwenye vyanzo vya maji, zoezi hili lilianza (2016) lakini kutokana na matatizo ya kifedha lilishindwa kumalizika. Mheshimiwa Theresia Ameomba wizara pia kusakafia mifereji inayotiririsha maji mang’ola. Mifereji iliyosakafiwa haifiki hata km 10 amesema mang’ola  kuna  km 80.3 za mifereji ambazo hazijasakafiwa, amesema kama wilaya wako tayari kufanya budget reallocation. Amewaomba wakulima wa mang’ola kuanza kuweka fedha kwenye mfuko kwa ajili ya kusakafia mifereji hiyo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa