• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DKT. MUSTAFA; WAFANYAKAZI WA AFYA, RUKSA KUJIENDELEZA KIELIMU

Posted on: May 26th, 2019

Maadhimisho ya siku ya wauguzi yaliyofanyika katika kituo cha afya Mbuga Nyekundu, yamefanyika kwa ufanisi mkubwa. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni wauguzi mbiu inayoongoza afya kwa wote.

Dkt. Mustafa Waziri amesema Karatu inawatumishi wa idara ya afya 356 kati ya 746 wanaohitajika kuna uhaba wa watumishi 390 wa idara ya afya. Amesema idara ya afya ina 52 % ya upungufu wa watumishi na ina 48% idadi ya watumishi walioajiriwa. Dkt Mustafa amesema  kuna changamoto kubwa ya watumishi, lakini bado idara ya afya inaendelea kupambana kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi.

Dkt.Mustafa amesema amekuwa akitekeleza zoezi la kuhamisha watumishi ili kukidhi mahitaji ya huduma kwa wananchi, amesema kwa sasa kila kituo cha afya kina watumishi wasiopungua watatu.Dkt  Mustafa, amesema anaendelea kulipa madai ya watumishi wa kada ya uguzi, amesema watalipwa kwa awamu na awamu hiki kiasi cha milioni 5 na laki 8 kinachodaiwa na wauguzi kitalipwa. Fedha hizo ni laki 1 na 20 elfu kama fedha za sare za kazi. Dkt. Mustafa amesema kwa watumishi wanaotaka kujiendeleza kimasomo kuna utaratibu mzuri wa kujiendeleza ili mradi mfanyakazi afuate utaratibu huo na yeye kama Mganga mkuu wa wilaya ataridhia. Amesema swala la motisha; kila kituo  kipange motisha kwa watumishi wake, amesema asilimia 15 ya makusanyo yanayofanywa kwenye kituo ya fedha yanabaki kwenye kituo na hilo lipo kwenye miongozo. Lakini pia kwa watumishi wanaokaa   mbali kama Matala watatumia gari la kituo cha afya Mbuga Nyekundu kuja mjini wanapokuja kuchukua mshahara. Amesema idara ya afya imewapa pikipiki  watumishi wa Matala na Ginamilanda.

Dkt, Mustafa amesema bado wanaendelea kutatua changamoto za nyumba za makazi za watumishi wa afya. Amesema  zahanati ya Endesh, kulikuwa na mtumishi alikuwa ameweka makazi ndani ya zahanati amesema mwezi huu ni wa mwisho kwa mtumshi huyo kuendelea kuishi pale.Diwani wa kata ya Baray kwa kushirikiana na Mganga mkuu wa wilaya wamemtafutia nyumba mtumishi huyo katika nyumba za makazi za wafanyakazi kwenye moja ya shule. makazi ya nyumba wamepewa pia watumishi wengine wawili waliopangiwa katika zahanati hiyo. Amesema idara ya afya iliweka bajeti ya million 10 ya kujenga nyumba kwa kushirikiana  na wananchi, Dkt Mustafa ameshukuru mkuu wa wilaya kwa kuweka mkazo kwa fedha hizo kwenda katika zahanati hiyo. Idara ya afya imeendelea kuwapandisha vyeo na kuwabadilishia muundo wa utumishi wafanyakazi wake.amesema kuna watumishi takribani 53 wamebadilishiwa mshahara na watumishi 9 wamebadilishiwa muundo wa Utumishi.

Wafanyakazi wa Idara ya afya wakiwa na nyuso za furaha kwenye maadhimisho ya siku ya wauguzi kituo cha afya Mbuga Nyekundu.

wauguzi wa Afya wakiwa kwenye maandamano katika sherehe za siku ya wauguzi zilizofanyika Mbuga Nyekundu.

Matukio mbalimbali ya maandamano ya siku ya wauguzi yaliyofanyika kituo cha afya Mbuga Nyekundu.

Picha za matukio mbalimbali wakati wa maandamano ya wauguzi kituo cha afya Mbuga Nyekundu.


Picha za mabango tofauti katika maadhimisho ya siku ya wauguzi kituo cha afya Mbuga Nyekundu.


Picha ya bango ikionyesha kauli Mbiu ya siku ya wauguzi, iliyofanyika kituo cha afya Mbuga Nyekundu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa