• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

RC, AHIMIZA KASI YA UJENZI HOSPITALI YA WILAYA

Posted on: February 16th, 2020

Mkuu wa mkoa wa Arusha ametembelea eneo linalojengwa hospitali ya wilaya ya Karatu, ziara hiyo ililenga kujionea maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya wilaya pamoja na kupata taarifa ya ujenzi wa hospitali.

Ujenzi wa hospitali ya wilaya ya karatu ulianza baada ya wilaya kupokea kiasi cha shilingi 500,000,000.00 kutoka mamlaka ya hifadhi ya Ngorongo. Halmashauri ilitenga kiasi cha shilingi 32, 000, 0000.00 kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Mpaka sasa mradi una majengo matatu , jengo la utawala na jengo la maabara yapo katika hatua ya lenta na jengo la wagonjwa wa nje limeshaezekwa  majengo. Mhe Mrisho Gambo amesema kuna kulegalega kwenye usimamizi wa ujenzi wa hospitali ya wilaya. Ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa wilaya ya Karatu kuongeza usimamizi katika ujenzi wa hospitali.  Mhe. Gambo amesema Mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro imeahidi kutoa million 100 kwa mwaka huu wa fedha kukamilisha jengo la maabara na jengo wagonjwa wa nje.

Ameongeza kusema Serikali pia imetoa milioni 500 nyingine kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya, fedha ambazo zinatarajiwa kutumika kuongeza idadi ya majengo katika ya hopitali ya wilaya. Wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI ilichelewa kupata taarifa za maendeleo ya ujenzi wa hospitali ya wilaya. Amesema fedha zilizotolewa na wizara ni kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala jengo la wagonjwa wa nje na jengo la maabara na tayari ujenzi ulishafanyika na umefikia katika hatua mbalimbali. Ametoa maelekezo kwa Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi wa Halmashauri kuandika barua ya clarification kwa wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa juu ya ujenzi wa majengo hayo matatu ambayo yameshajengwa.  Ili million 500 za serikali zilizotolewa zijenge majengo mengine badala ya hayo matatu, amesema hospitali ya wilaya inapaswa kuwa na majengo saba.

Naye Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe.Theresia Mahongo amesema atafuatilia kuhakikisha ujenzi wa hospitali ya wilaya unakamilika kwa wakati. Amesema atatumia wahandisi wa ujenzi wa Tarura ili kupata ushauri wa kitaalamu hasa katika ujenzi wa majengo hayo mapya yanayotarajiwa kujengwa. Mhe. Mahongo amesema wananchi watajitolea nguvu kazi ya kujenga msingi kwa majengo hayo mapya yanayotarajiwa kujengwa. Ameomba serikali kuharakikisha kutoa million 500 ili waweze kuhakikisha ndani miezi mitatu ujenzi wa majengo uwe umekamilika. Mhe. Mahongo ametoa salamu za shukurani kwa niaba ya wananchi wa wilaya ya Karatu kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu Mhe Emmanuel Gege amesema swala la ujenzi wa Hospitali ya wilaya litakuwa ajenda kuu kwa sasa. Amesema yeye kama muwakilishi wa wananchi atashirikiana na watendaji kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati. amesema watatumia pia mawazo mbadala  kuhakikisha ujenzi unaenda haraka, Mhe. Gege ameshukuru viongozi kwa kulisimamia kidete swala la ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Picha ni Muonekano wa nje wa jengo la wagonjwa wa nje baada ya kuezekwa 

Mkurugenzi Mtendaji ndugu Waziri Mourice amesema watendaji wa Halmashauri wamefikiria kutumia fedha za ndani million 40 kukamilisha majengo mawili ya maabara na jengo la wagonjwa wa ndani. Amesema watendaji watatumia uadilifu kukamilisha mradi wa ujenzi na kuhakikisha wanasimamia vizuri matumizi ya fedha za ujenzi wa majengo hayo mawili ili yaanze kutumika ifikapo mwezi wa saba mwaka huu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa