• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SABABU; VIFO VINAVYOTOKANA NA UZAZI , WATOTO WACHANGA ZINAZUILIKA

Posted on: August 2nd, 2019

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo amezindua kampeni ya “jiongeze, tuwavushe salama tupunguze  vifo  vitokanavyo na uzazi. Uzinduzi huo umefanyika katika ukumbi wa Halimashuri ya wilaya ya Karatu na ulihudhuriwa na wadau mbalimbali wa afya.

 Mhe. Theresia amewapongeza sana wafanyakazi wa sekta ya afya kwa kuendelea kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. Ametoa wito kwa wakunga wa jadi kuendelea kushirikiana na watendaji wa afya wa serikali na kuendelea kuwahamasisha kina mama wajawazito kuhudhuria vituo vya afya. Amesema lengo letu ni kuhakikisha wakina mama wanajifungua salama  na kupunguza vifo vinvyotokana na uzazi. Amesema serikali imeongeza fedha ktika idara ya fedha ili kinamama watarajiwa na watoto wa umri chini ya miaka mitano wapate huduma ya afya bure. Amewapongeza wadau wa afya wanaoshirikina na serikali, amesema kazi inaoenekana na natambua mchango wenu katika kuimarisha afya ya mama na mtoto. Amewaomba kuzidi kushiriki katika kuongeza rasilimali zote muhimu zitazolenga kuboresha afya ya mama na mtoto katika wilaya ya karatu.

 Mhe. Theresia ametoa wito kwa Maafisa tarafa, kusimamia hatua zote muhimu ili kupunguza vifo vya uzazi na watoto wachanga. Amesema kila mtendaji afanye ajenda ya afya ya mama na mtoto kuwa ajenda muhimu katika vikao vyake. Amesema ni matumaini kwamba maafisa tarafa watafuatilia kwa umakini taarifa za afya kwa ngazi zote ndani ya tarafa ili taarifa za kinamaa wajawazito na watoto wachanga ziwekwe na kutunza vizuri. Maafisa tarafa wamesaini hati ya kiapo ya kutekeleza majukumu hayo mbele ya mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo na kaimu mkurugenzi Mtendaji wa wilaya, ndugu Godfrey Luguma.

Amesema sababu nyingi za vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto wachanga zinazuilika, ndio maaana tunahamasisha jamii itoe elimu ya afya ikiwa pamoja na kuhamasisha wananchi kupenda kuhudhuria kiliniki. Mhe. Theresia amesema kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi ni swala mtambuka amehimiza ushirikishawaji viongozi wa dini, viongozi wa vijiji vitongoji na madiwani ili kusaidia kuhamisha wakinamama wajawazito kupenda kuhudhuria hospitali.

 Awali katika taarifa yake Mganga mkuu wa wilaya Dtk Musatafa Waziri amesema kuna ucheleweshaji wa mama mtarajiwa ngazi ya jamii. Amesema wakinamama wajawazito huwa wanajifungulia nyumbani hawafiki vituo vya kutolea huduma mapema. Amesema kuna swala la mila ambalo linafanya mama mtarajiwa kutokuwa na maamuzi ya kwenda hospitali, au kutumia dawa za kienyeji badala ya kufika hospital au kituo cha afya. Jambo linalosababisha mama kupata uchungu kabla ya muda; wakati mwingine  kupoteza damu nyingi wakati wa kujifungua jambo linalosababisha kifo. Amesema kuna swala la umbali wa vituo hasa katika huduma za upasuaji nayo imekuwa moja ya changamoto ya kukabiliana na vifo vya uzazi. Amesema swala hilo pia linahusisha ubovu wa barabara hasa wakati wa masika na uhaba magari katika vituo vya afya. Amesema vituo vya afya Mbuga nyekundu, Kambi ya simba vina magari lakini Oldean bado hakuna gari. Amesema wanaendelea kukarabati jengo la upasuaji (theater) Mbuga nyekundu na kituo cha afya Endabash upasuaji utaanza mwezi wa kumi mwaka huu. Dkt Mustafa amesema ucheleweshaji ndani ya vituo, kwa mama mjamzito kupata huduma nayo imekuwa ni sababu ya vifo vya uzazi. amesema kunasababishwa na kukosekana kwa vifaa, kukosekana kwa mtoa huduma katika vituo vya afya au uzembe kwa watoa huduma. Taarifa zote za vifo za  vinavyosababishwa na uzazi zinaripotiwa na zinajadiliwa ndani ya muda wa saa 48 ili sababu zilizosababisha zisijitokeze tena.

Dkt. Mustafa amesema sababu hizo tatu ndio lengo la kuzindua kampeni ya “JIONGEZE, TUWAVUSHE SALAMA TUPUNGUZE VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI” . Dkt. Mustafa amesema hakuna tatizo la benki ya damu, amesema Karatu inaongoza kwa uchangia chupa 1250 kwa mwaka uliopita. Amesema hakuna kituo chchote cha afya kinachouza damu kwa mgonjwa. Amesema mwaka huu vifo vya kinama kuanzia January mpaka mwezi wa June, vifo vya wazazi ni viwili na vifo vya watoto wachanga vilikuwa 11. Dkt. Mustafa amesema wao kama wadau wa afya wanajitahidi kupunguza vifo hivyo, ndio maana wamezindua kamapeni hiyo.    

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa