• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SABATO WAUNGA MKONO MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Posted on: April 15th, 2020

Na Tegemeo Kastus

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Theresia Mahongo amepokea mchango wa fedha kutoka kwa viongozi wa kanisa la sabato Karatu.  Michango hiyo imetolewa baada ya Mkuu wa wilaya kuhamasisha wadau kuchangia michango ili kununua vifaa tiba vya kukabiliana na tishio la ugonjwa (COVID-19) virusi vya corona.

Mhe. Mahongo ameshukuru wachungaji wa kanisa la sabato kwa msaada wa fedha kiasi cha Tsh 1,510,000 utakaotumika kununua vifaa mbalimbali vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona. Mhe. Mahongo amesema kanisa la KKT Karatu nalo linatarajia kutoa kiasi cha Tsh 1,000,000 kwa ajili ya kununua vifaa vya kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya corona. Mhe. Mahongo ameshukuru wadau wote wanaoendelea kuchangia vifaa kwa ajili ya kukabiliana na janga la ugonjwa wa virusi vya corona.

 Mhe. Mahongo amesema wameshapokea vifaa vingine vichache kutoka kwa wadau wengine ambavyo ni mabuti, kuna wadau waliochangia (mask) barakoa, wadau wengine wamechangia gloves, kuna wadau waliochangia fedha kiasi cha Tsh. 600,000 mpaka wakati  anakutana na viongozi hao wa kanisa la sabato.

Mhe. Mahongo amewahakikishia viongozi wa kanisa la Sabato kwamba fedha zilizotolewa zitatumika vizuri na mchanganuo wa matumizi yake utawekwa wazi. Amesema fedha hizo zitaenda kununua vifaa ambavyo waliomba siku za awali  na vitafanyia kazi ambayo inatarajiwa kufanywa. Mhe Mahongo amesema ofisi ya Mkuu wa wilaya itatoa barua ya kuwatambua wadau kwa mchango wao.

Mhe. Mahongo amesema daktari aliyemhudumia mgonjwa ambaye baadae alibainika ana virusi vya corona huko Longido alikuja Karatu. Tayari mshukiwa huyo amechukukuliwa na kupelekwa Arusha  kwa uangalizi (karantini) na nyumba ya wageni aliyofikia  Karatu imewekwa karantini. Mhe. Mahongo amesema watu watatu wako chini ya uangalizi (wamewekwa karantini)  na ufuatilia unaendelea ili kujua mganga huyo amekutana na watu wangapi (contact tracing).

Mhe. Mahongo amesema tunafanya hivyo ili kuendelea kujikinga, amesema wahudumu wa nyumba za wageni walishapewa maelekezo kuendelea  kujihadhari kwa kuvaa (mask) Barakoa na gloves wakati wa kuhudumia watu ili kujikinga na maambukizi.

Mkuu wa wilaya Mhe. Theresia Mahongo  akiwa katika kikao na viongozi wa kanisa la sabato Karatu kilichofanyika katika ofisi ya mkuu wa wilaya.

Mchungaji Dikson Mkama wa kanisa la Sabato Karatu amesema wametambua kazi ya kukabiliana na ugonjwa wa virusi vya corona ni kazi ngumu. Amesema baada ya kikao cha wadau Mchungaji Mkama alipeleka wito kwa waumini kanisani na kuhamasisha waumini wachangangie na kuunga mkono jitihada za serikali za kupambana na corona.  Amesema waumini wamelipokea swala hilo kwa uzito mkubwa ndio maana wamewakilisha mchango wa waumini ofisi ya Mkuu wa wilaya kama sehemu ya jitihada zao za kupambana na vita dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa corona.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa