• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SAKATA LA UJENZI WA SOKO KARATU LACHUKUA SURA MPYA

Posted on: August 30th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo ameendelea na ziara yake wilayani Karatu. Ziara hiyo iliyoingia katika siku ya nne ametembelea soko la kuu la Karatu, ambalo ujenzi wa kuezeka bado unaendelea.

Mhe. Gambo amesema haridhishwi na kasi ya ujenzi wa soko kuu la mjini Karatu, ujenzi wa soko hilo ulianza mwezi 30/5/2018 na kutarajiwa kukamilika mwisho wa mwezi wa 8 mwaka 2018. Amesema tayari miezi mitatu iliyokusudiwa imeshaisha na sasa mwaka umepita, wananchi wameendelea kujibana kwa muda katika maeneo yasiyo rasmi kwa biashara wakitegemea serikali iwatengenezee  maeneo mazuri zaidi ya kufanya biashara.

Mhe. Gambo amesema kitendo cha jengo hilo kutumia mchoro wa ramani ya pili baada ya ile ramani ya kwanza kimeonesha mapungufu ya kiutaalam. Amesema dosari hiyo imeweka mashaka juu ya uwezo wa mhandisi wa wilaya katika utendaji kazi. Mhe. Gambo amemuelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya karatu kumuondoa katika nafasi yake mwandisi huyo na kutafuta mhandisi mwingine kujaza nafasi yake kwa kushirikiana na katibu tawala wa mkoa.

Mhe. Gambo amesema mtu wa manunuzi wa Halmashauri, naye pia hajaweka mbele maslahi ya umma na wamefanya uzembe katika utendaji kazi. Mhe. Gambo amesema Halmashauri imelipa fedha bila kuona vifaa vinavyonunuliwa, utaratibu unaagiza vifaa na vifaa vikishafika vinakaguliwa na mkiridhika mnalipa. Halmashuri imelipa zaidi ya million 100 na vifaa vingine bado havijafika eneo la ujenzi. Amesema bado hata vifaa vilivyofika wataalam wamekiri vilikuwa na matatizo hivyo kurudishwa tena. Ametoa maelekezo ya kusimamishwa kazi kwa afisa manunuzi na kumuelekeza katibu tawala wa mkoa kuuunda timu ya uchunguzi katika ujenzi wa soko kuu la mjini Karatu. Mhe. Gambo ametoa muda mpaka 15/10/2019 soko kuu la Karatu liwe limekamilika kabisa na kuanza kutumika.

Awali katika taarifa yake mbele ya mkuu wa mkoa mhandisi Venance Malamla amesema mradi huo wa ujenzi wa soko ulikadiriwa kutumia million 540. Halmashauri kutokana na upungufu wa fedha imegawa ujenzi wa soko katika awamu mbili, awamu ya kwanza itagharimu shilingi million 222. Mhandisi Malamla amesema katika awamu hiyo ujenzi ulihusisha nguzo na kupauwa jengo lote. Hatua ya pili ya ujenzi ni kujenga sakafu; vizimba, kujenga ukuta wa nje na kuweka miundo mbinu ya maji na moto. Utaratibu wa kujenga soko hilo unatumia force account, mradi huo unatekelezwa na fundi Anatory construction limited akiletewa vifaa na kusimamiwa na wataalamu wa Halmashauri.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa