• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SEKTA YA AFYA MSIPOJIPANGA, MTAPANGWA

Posted on: April 9th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Vituo vingi vya afya vimekuwa na tabia ya kutotoa huduma siku ya Jumamosi na Jumapili jambo linalosababisha adha kubwa kwa wananchi. Sasa  uwekwe utaratibu mzuri ili mgonjwa anapokuja kupata huduma aweze kusikilizwa kwa wakati kwa sababu ugonjwa hauna muda maalumu. Kila kituo cha kutolea huduma kiwe na bango la namba za viongozi ili ikitokea changamoto mgonjwa kukosa huduma aweze kutoa taarifa.

Hiyo itasaidia wananchi kufikisha kero zao za kukosa huduma kwa wakati ili ziweze kutatuliwa bila kupata adhaa. Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea zahanati ya Qurus na zahanati ya Gongali katika ziara yake ya kuangalia upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya wilaya ya Karatu. Mh. Kayanda amebaini utoro kwa baadhi wa watumishi wa afya, kuondoka vituo vya afya hasa siku za mwisho wa juma bila ya kuwa na sababu maalumu jambo ambalo linalochangia kudhorotesha hali ya utoaji wa huduma.

Mh. Abbas Kayanda akikagua hali ya utoaji wa huduma katika zahanati ya kijiji cha Gongali kata ya Qurus

Mh. Kayanda amebaini udhaifu wa kutokuweka mazingira ya kutolea huduma za afya katika hali ya  usafi jambo ambalo linatoa taswira mbaya ya utoaji wa huduma za afya. Ameelekeza waganga wasimamizi kuhakikisha wanaweka katika hali ya usafi vituo vya kutolea huduma na kuhakikisha  hali ya usafi inaimarika kwenye vituo vya kutolea huduma ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vifaa tiba vinavyohitajika katika utoaji wa huduma vinapatikana. Ameongeza kusema rejista ya utoaji wa dawa lazima ijazwe ili kujua dawa zilizoingia na dawa zilozotoka. Mh. Kayanda amesema katika vituo vyote alivyotembelea amebaini upotevu wa madawa ambao umechangiwa kwa kiasi kikubwa na udhaifu wa kujaza  rejista ya dawa hivyo kutoa mwanya wa dawa za serikali kupotea. Katika ziara hiyo Mh. Kayanda ametoa maelekezo mahususi kwa mganga msimamizi wa  zahanati ya Qurus kuhakikisha  dawa zote zinaingia kwenye rejista baada ya kukuta zahanati ya Qurus rejista yake ya dawa haijajazwa tangu mwaka jana 2020 na MSD wameleta dawa mwaka huu ambazo nazo hazijaingia kwenye  kwenye rejista na wala hazijapangwa kwenye chumba cha dawa.

Mh. Kayanda akimjulia hali mama aliyekuja kupata huduma ya afya katika zahanati ya Gongali

Mh. Kayanda amebaini uzembe wa mganga wa zahanati ya Qurus kutokuwa na chanjo ya polio jambo lilosababisha zahanati hiyo kushindwa kutoa chanjo ya polio kwa watoto wadogo. Amemueelekeza mganga msimamizi wa zahanati hiyo kuhakikisha jumamosi amepata chanjo ya polio katika kituo chake cha kutoa huduma na kuitoa kwa watoto. Ikiwa ni sambamba na kugawa vyandarua kwa kinamama wenye watoto wa changa na kuhakikisha hakuna mwananchi anayeenda kununua dawa kwenye maduka binafsi kwa sababu dawa zinaletwa na serikali.

Katika hatua nyingine Mh.Kayanda amemuelekeza Mganga Mkuu wa wilaya kuandika barua bohari ya madawa MSD ili kuhakikisha wakati wa usambazaji wa dawa kwenye vituo na zahanati kamati za dawa za vijiji  zinashirikishwa kikamilifu katia makabidhiano. Amesema hiyo itasaidia kamati za dawa kujua ni dawa kiasi gani zimeletwa katia kituo cha afya ili viongozi wa kamati watoe taarifa kwa wananchi. Badala ya mtindo wa sasa ambao hauendani na sera ya afya ambao watu wa bohari ya dawa wanakabidhi dawa kinyemela kwa wahudumu wa afya peke yake.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa