• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI KUSIMAMIA HAKI YA NG’OMBE ZILIZOULIWA BUGER

Posted on: November 4th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Timu maalumu ya uchunguzi itakayohusisha Maafisa wa Tanapa ziwa Manyara na vyombo vya ulinzi na usalama itafanyaa uchunguzi wa ng’ombe wa tatu waliouliwa kwa kupigwa risasi. Ili kufahamu undani wa ng’ombe waliouliwa ulifanyika ndani ya hifadhi au nje ya hifadhi ya ziwa Manyara.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Buger katika mkutano wa hadhara. Amesema timu ya uchunguzi itakapokuja lazima ije iripoti kwa Uongozi wa kijiji cha Buger, ili iweze kupata ushirikiano wa viongozi na wananchi wa Buger. Uchunguzi utakapodhibitisha kwamba askari wamechukua maamuzi nje ya utaratibu, hatua  za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao ili iwe fundisho kwa askari wengine  wenye tabia kama hizo kuacha kujichukulia maamuzi nje ya utaratibu.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na wananchi wa Buger katika mkutano wa hadhara

Mh. Kayanda amekemea pia tabia ya askari wa hifadhi kuvamia makazi ya watu nyakati za usiku amesema huo siyo utaratibu mzuri. Amesema kama kuna mtu amekosea, utaratibu wa kisheria lazima uendelee kufuatwa. Kuvamia mtu usiku ni hatari kwa askari mwenyewe lakini  hata kwa mwananchi inafanya watu wanaishi kwa hali ya wasiwasi. Wananchi wanapaswa kuwa huru kufanya shughuli zao katika kijiji kwa amani halikadhalika askari wa hifadhi nao wako huru kufanya kazi zao.

Mh. Kayanda amewaomba wananchi kuendelea kuheshimu makubaliano yaliofikiwa mwaka jana kati ya wananchi na viongozi wa hifadhi ya ziwa Manyara kuhusiana na kutoingiza  mifugo kwenye hifadhi. Amesema hifadhi ikivamiwa na kila mtu, mwisho wa siku kutakuwa hakuna hifadhi, na itakuwa ni hasara kwa nchi yetu. Moja ya mambo walikubaliana ni pamoja na kutoza faini Mifugo itakayokamatwa  ndani ya hifadhi kwa mujibu wa sheria, na kuendelea kuishi kwa amani na upendo kati maskari wa hifadhi ya ziwa manyara na wananchi wanaoishi kuzunguka hifadhi ya ziwa Manyara.

Naye Kamishina Msaidizi wa Tanapa Ndg. Herman Batiho amesema sheria inamtaka mtu anayetaka kuingia kwenye hifadhi kupata kibali cha wenye mamlaka. Sheria za hifadhi haziruhusu mtu kufanya shughuli zozote za kibinadamu ndani ya eneo la hifadhi, ikiwa ni pamoja na uwindaji, kukata miti na kulisha mifugo. Amesema mtu anayebainika kufanya mambo kama hayo  sheria imeweka wazi kiasi cha faini kilichopitishwa na bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Mh. Abbas Kayanda katika matukio tofauti wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Buger

Kamishina Msaidizi ndg. Batiho akizungumzia tukio la kuuawa ng’ombe lilofanyika, amesema hakuna kiongozi wa  hifadhi aliyeelekeza askari kufanya tukio kama hilo. Askari wamepewa vitendea kazi vya kufanya kazi ya kulinda hifadhi amesema baada ya tukio hilo lilojitokeza ni vizuri kupata chanzo cha tatizo hilo kwa kuunda timu ya uchunguzi na ikibainika mshukiwa achukuliwe hatua za kisheria na kiutumishi zitachukuliwa na TANAPA.

Mama mwenye mifugo iliyouliwa Bi, Roziana Emmanuel amesema ng’ombe wake walikuwa kwenye malisho shambani kwake nyumbani mida ya saa tano asubuhi, kabla ya kuuwawa na askari wa hifadhi. Bi, Roziana amemuomba mkuu wa wilaya ya Karatu kusimamia changamoto hiyo ili iweze kutatuliwa.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa