• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SERIKALI YAZIDI KUIMARISHA MIUNDO MBINU YA ELIMU

Posted on: September 14th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Watendaji wapewa wito wa kutumia rasilimali vizuri katika kusimamia ujenzi wa miradi ya maendeleo inayojengwa katika maeneo yao. Serikali imeweka matumizi ya force acount ili kusaidia thamani ya miradi ya ujenzi iendane na kiasi cha fedha zilizotolewa kushirikiana na kamati ya usimamizi wa  ujenzi.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea ujenzi wa miundo mbinu ya elimu na kupokea taarifa ya vyumba vya madarasa katika shule za sekondari za Domel, Baray na Mang’ola kulingana na matarajio ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza. Sambamba na hilo ametembelea miradi ya ukamilishaji wa maabara katika shule ya sekondari Domel na Mang’ola . shule hizo zimepewa kiasi cha shilingi million 30 kila moja kwa ajili ya ukamilishwaji wa maboma ya maabara ya somo la kemia. Mh. Kayanda ameoneshwa kuridhishwa na ujenzi wa miundo mbinu ya maabara ya sekondari hizo. Amepongeza Mkuu wa shule ya sekondari Mang’ola kwa usimamizi mzuri kwa kushirikiana na kamati ya ujenzi kuweza kubaki  kiasi cha shilingi million 4, kiasi ambacho tayari kimeombewa kibali kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Karatu kwa ajili ya kutumika  kupiga plasta katika majengo mengine ya mabara ya fizikia na bailojia.

Mh. Kayanda akiwa katika jengo la maabara ya sekondari Domel.

Mh. Kayanda ametembelea shule ya sekondari Baray ambayo serikali za vijiji vinne vinavyozunguka shule hiyo vimekubaliana kujenga na kuinua maboma mawili ya madarasa kwa ajili ya kukabiliana na upungufu wa madarasa. Mh. Kayanda amepongeza jitihada za Halmashauri ya vijiji hivyo, huku Halmashauri ya wilaya ya Karatu ikitenga katika mwaka huu wa fedha kiasi cha million 10 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametembelea shule ya msingi Qangnded iliyopewa kiasi cha million 40 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa  kupitia mfuko wa EP4R. Huku kiasi kingine cha million 19 kimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo katika shule hiyo. Mh. Kayanda amehimiza wakandarasi kumaliza kazi hiyo kwa mujibu ya muda ulioainishwa kwenye mkataba, na kuhakikisha ujenzi wa miundo mbinu ya vyumba vya madarasa unaendana na thamani ya fedha iliyotolewa.

Muonekano wa jengo la maabara ya kemia kwa nje shule ya Mang'ola sekondari.

Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha mazingira ya kujifunza na kufundishia yanazidi kuimarika, na kujikita katika kuondoa daraja sifuri. Huo ni mkakati wa wilaya na ni mkakati wa serikali kupitia wizara ya Tamisemi kuhakikisha hakuna ufaulu wa daraja sifuri. Amesema ili kupigania mkakati huo lazima mwanafunzi atimize wajibu wake wa kusoma kwa bidii na kuzingatia masomo anayofundishwa darasani, na mwalimu amupe mwanafunzi mbinu na maarifa ya kitaaluma ili mwanafunzi aweze kufaulu mtihani. Wakati huo huo mzazi atimize wajibu wa kumpatia mahitaji mwanafunzi na kusimamia vizuri katika malezi na ustawi wake wa kitaaluma.

 Mh. Kayanda alipotembelea zahanati ya Mang'ola barazani kujionea hali ya utoaji huduma za afya.

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametembelea zahanati ya Mang’ola Barazani ambayo wadau wa maendeleo shirika la world vision limeahidi kufanyia ukarabati jengo la mama na mtoto katika zahanati hiyo. Mh. Kayanda ametoa rai kwa mkandarasi kuanza kazi ya ukarabati mapema ili kuboresha miundo mbinu ya zahanati hiyo. Mh. Kayanda  amekagua hali ya upatikanaji wa dawa katika zahanati hiyo ya Mang’ola barazani na amehimiza wahudumu wa afya kubandika kwenye vituo vyao vya afya aina za dawa zinazopatikana ili wananchi waweze kufahamu. Amehimiza watendaji wa afya kufuata taratibu za kuweka na kutoa dawa kwa kuhakikisha  wanajaza kitabu cha rejesta ya dawa.

picha katika matukio tofauti wakati Mh. Kayanda alipotembelea zahanati ya Mang'ola barazani.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa