• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SHIDA YA MAJI GETAMOCK, SASA BASI !!!

Posted on: March 31st, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Mradi wa maji wa Getamock ulioshindwa kufanya kazi kwa muda miaka zaidi ya nane, sasa umeanza kufanya kazi. Mradi huo uko chini ya uangalizi wa ruwasa na una vituo vya kutolea maji ishirini na sita ambavyo vimeanza kutoa maji katika kata ya Endamarariek.

Hayo yamebainika katika ziara ya mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea kata ya Endamariek kukagua shughuli za maendeleo. Mh. Kayanda amesema ni wakati sasa wa jumuiya za watumia maji kusimamia miradi huo vizuri ili uweze kuleta manufaa kwa wananchi. Ameongeza kusema fedha za makusanyo ya huduma ya maji ziwekwe katika akaunti ya jumuiya ya watumia maji Getamock ili kuepusha watu kutumia fedha mbichi. Fedha hizo ndizo zitasaidia kurekebisha miundo mbinu ya maji na kusaidia mradi kujiendesha.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika dp ya maji katika kijiji cha Getamock

Mh. Kayanda ametoa mda wa siku tisa ili fedha zote zilizokusanywa ziwe katika akaunti iliyofunguliwa na jumuiya ya watumia maji Getamock. Wakati huo huo Mh. Kayanda amemuagiza mkaguzi wa ndani kufanya ukaguzi wa fedha hizo ili kujiridhisha kama hakuna ubadhilifu uliojitokeza.

Mh. Kayanda ameomba wananchi kuheshimu wataalam wa fedha watakaokuwa wanasaidia kusimamia mapato na matumizi ya fedha katika jumuiya ya watumia maji. Lengo ni kusaidia shughuli za fedha kuendeshwa kitaalamu kulingana na sera na miongozo ya serikali. Amesema usimamizi wa maji utakuwa mzuri, na utajenga utamaduni wa kutoa taarifa za mapato na matumizi. Miradi ya jamii lazima iendeshwe kwa uwazi na huo ndio utendaji kazi mzuri. Mh. Kayanda amepongeza wakala wa maji vijijini kwa jitihada walizofanya za kufufua mradi wa maji. Amesema matokeo sasa yanaonekana hii inatokana na juhudi za serikali za kuiweka miradi ya maji chini ya wakala wa maji vijijini.

Mhandisi Baraka Kilangai akimueleza Mh. Abbas Kayanda namna mfumo wa maji utakuwa unavyofanya kazi.

Mh. Kayanda amekemea tabia ya watu wasio waaminifu kuhujumu miundo mbinu ya maji, ameelekeza uongozi wa kijiji kusimamia na kulinda kikamilifu miundo mbinu ya maji. Lazima tujenge nidhamu ya kulinda rasilimali za maji, kwa mtu mmoja mmoja kuwajibika kusimamia usalama wa miundo mbinu ya maji ili kukomesha tabia za kukata kata mabomba ya maji.

Naye wakala wa maji vijijini Ruwasa Mhandisi Baraka kilangai katika taarifa yake amesema wakala wa maji vijijini wamerekebisha km 8.9 kati ya km 14 zinazotakiwa kurekebishwa. Amesema katika kipindi cha matazamio walichojiwekea maji yanatoka vizuri japokuwa kuna wakati maji yanatoka kwa kusuasua. Mhandisi Kilangai amesema mkakati wao ni kuhakikisha wanamalizia sehemu ambazo hawajazifanyia marekebisho ili watu wapate maji bila kuwa na changamoto yoyote.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa