• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SHIRIKA LA JIVITA LATOA TAULO ZA KIKE 1632

Posted on: September 27th, 2019

Shirika lisilo la kiserikali la (JIVITA) Jitegeeme vijana Tanazania foundation; limetoa taulo za  kike kwa  vijana wa kike walio shuleni katika wilaya ya Karatu. Msaada huo ni jitihada za kumsaidia mtoto wa kike kutimiza ndoto zake.

Bi, Yasinta Lekule Afisa vijana wa Jivita; amesema katika mradi wa kugawa taulo unaoitwa Mwanao, wameweza  kusambaza taulo za kike 1632 ndani ya wiki moja kwa shule 9 za serikali wilayani Karatu. Bi Yasinta amesema kila mtoto amepata taulo moja na lengo ni kusambaza taulo kwa vijana walio shuleni wenye uhitaji. Zoezi hilo limefanyika katika ukanda wa kata ya Kansay Tarafa ya Endabash na baadhi ya shule katika tarafa ya Karatu. Amesema lengo la shirika hilo ni kutoa msaada kwa wilaya nzima, awali walianza zoezi hilo kwa kugawia vijana wa kike katika tarafa ya Eyasi.

Bi, Yasinta amesema, “lengo ni kumwezesha mtoto wa kike kutimiza ndoto zake.” Kijana wa kike lazima ajisitiri vizuri wakati anasoma. Amesema vijanawa kike wenye uhitaji hukosa masomo kwa kutohudhria shule kwa kuhofia kuadhirika pindi wanapokuwa kwenye mzunguko wa hedhi.Amesema zoezi hilo ni endelevu na wanatarajia kuja mwezi wa kumi kusaidia tena vijana wenye uhitaji.

Shirika linajihusisha na Mradi wa Sio Mwisho, ambao nao umejikita katika kuwawezesha watoto waliokosa shule kwa kuwapatia huduma  muhimu. Bi, Yasinta amesema wana jihusisha na watoto waliokosa shule ambao wanaishi mtaani, wao kama Jivita wanawasaidia kurudi nyumbani na kuwashawishi kuendelea na masomo au kusoma kitu anachokipenda. Amesema wanafanya shughuli zote hizo kupitia wafanyabiashara wa mjini Arusha wanaotoa misaada mbalimbali kwa ajili ya vijana hao. Amesema kwa sasa wanafanya shughuli hizo katika mji wa Arusha, lakini wataongeza wigo wa kazi zao kwa wilaya nyingine.

Bi, Yasinta amesema shirika lao limejikita katika shughuli za mazingira, amesema mabadiliko ya nchi yanaathari kubwa sana katika shughuli za utalii. Shirika limezindua kamapeni ya Nitunze  Mazingira, Mazingira Yakutunze ambayo itazinduliwa mkoani Arusha 14/Oct/2019. Amesema kuelekea wiki ya kilele cha siku ya utalii; tumepanda miti 300 kwa kushirikiana na shirika la TAJPI kwa shule za serikali za sekondari na msingi. Amesema malengo yao ni kuzuia athari za kimazingira zinazochangiwa na utunzaji mbovu wa mazingira.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa