NA TEGEMEO KASTUS
Halmashauri ya wilaya ya Karatu imefanikiwa kukusanya 93% ya mapato ya kodi ya ndani kwa mwaka wa fedha uliopita. Kiwango hicho hakiwahi kufikiwa tangu Halmashauri ya wilaya ya karatu ilipoanzishwa.
Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu. Amesema Halmashauri imefika hapo kwa sababu ya team work. Mkurugenzi hawezi kufanya hizi kazi peke yake lazima apate ushirikiano na kutoka kwa wakuu wa idara na watumishi wengine wa ngazi za chini. Mh. Kayanda amesema kwenye maswala ya lishe na ICHF Halmashauri imeshika nafasi ya pili kwa ngazi ya mkoa. Amesema ufaulu wa elimu ya msingi umetoka wastani wa 65% mpaka kufikia 82.
Mkuu wa wilaya Mh. Abbas Kayanda akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Karatu
Mh. Kayanda amesema watumishi wanatakiwa wawe na maadili na wanatakiwa wayaishi Maadili ya utumishi wa umma nje na ndani ya ofisi. Lazima watumishi wavae mavazi yanayoendana na maadili ya utumishi wa umma, amesema mtumishi anawajibika kutunza mali za serikali.
Mh. Abbas Kayanda akiwa anazungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu.
Mh. Kayanda amesema Migogoro ya ardhi iliyodumu muda mrefu lazima imalizwe, amesema hapendi kuona wananchi wakisumbuliwa kupata haki zao. Amesema lazima watumishi wote wawe kitu kimoja, ikitokea mtu mmoja anavuta kurudi nyuma atasababisha kurudi nyuma watu wote ikitokea mtu anavuta mbele atasababisha watu wote kwenda mbele. Amesema ushirikiano ni jambo la muhimu sana katika utendaji wa kazi, amesema ni vyema watu kufanya kazi kwa kuzingatia miongozo ya kazi.
Mh. Kayanda amesema kila mtumishi ana nafasi yake amesema hapendi kuona mtu anaonewa kwa sababu ya udogo wake katika kazi amesema mtu kama anaadhibiwa basi aadhibiwe kwa makosa aliyoyafanya. Amesema kama mtu anapongezwa apongezwe kwa sabababu ya ufanisi wake katika kazi. Amesema ni vizuri watumishi kuheshimu mipaka ya kazi na kuheshimu mipaka ya kazi ya watumishi wengine.
Karatu District Council
Sanduku la Posta: P.O Box 190
Simu: +255 272970648
Simu ya Mkononi: 0754773947
Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz
Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa