• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

TAARIFA ZA MAENDELEO ZA KATA ZAWASILISHWA

Posted on: April 29th, 2019

Kikao cha kawaida cha baraza la madiwani kimekaa leo katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu. Kikao hicho cha robo ya tatu ya mwaka kimeongozwa na Mwenyekiti wa baraza la madiwani Mhe. Jublate Mnyenye.

Kikao hicho kiliwapa nafasi waheshimiwa madiwani kutoa taarifa za maendeleo za kata kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Sambamba na hilo pia madiwani walihoji uhalali wa taarifa za kata, ambazo madiwani wao wamejiuzulu na hazikuwa na uwakilishi wa madiwani.

Mwanasheria wa Halmashauri Ndugu Prosper Ndomba alieleza mbele ya baraza la madiwani tafsiri ya kanuni kisheria. Kanuni ya ishirini na tano, kanuni ndogo ya pili inasema taarifa za utekelezaji wa kata zitawasilishwa na diwani wa kata husika, na kama diwani huyo hayupo itawasilishwa na diwani wa viti maalumu anayeishi katika kata hiyo, na kama diwani wa viti maalumu hayupo, Mwenyekiti atamtaarifu mapema diwani mwingine yeyote asaidie kuwasilisha taarifa hiyo. Ndugu Ndomba amesema taarifa zinaletwa ili kama kuna hoja au swala la ufuatiliaji liende kwenye kamati husika. Hakuna hofu ya kuwasilisha taarifa na wala muwasilishaji habanwi kujibu taarifa ya kata husika.

Mhe. Jublate ameomba waheshimiwa madiwani kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga katika mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa. Elimu iendelee kutolewa kwa wananchi wengi, ili wajitokeze kujiandikisha na wapate bima ya afya. Mhe Jublate amesema mambo yamebadilika  bima ya afya ni swala muhimu sana, gharama za matibabu zipo juu. Serikali hutoa msaada kwenye maeneo ambayo wamefika zaidi ya 25% ambayo serikali inachukulia kama kiwango cha chini. Amesema  ili serikali iweze kutoa top up ya 25% lazima tufike kiwango cha chini cha serikali. Mhe. Jublate amesema Karatu  haijafika kiwango cha 25% ili kuweza kunufaika na (top up ) fedha za serikali.


Waheshimiwa madiwani katika kikao cha baraza la madiwani.

watendaji wa Halmashauri katika baraza la madiwani.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa