• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

TAHOSSA WAHIMIZWA KUIMARISHA UMOJA WILAYANI

Posted on: February 26th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Wakuu wa shule za sekondari mkoa wa Arusha wamehimizwa kuimarisha umoja katika kufanya kazi katika maeneo yao ya kazi. Hiyo itasaidia kubadilishana uzoefu na kuongeza maarifa na weledi wa kuongoza shule na kuinua kiwango cha ufaulu wa wanafunzi.

Mh. Abbas Kayanda amesema hayo wakati akifungua mkutano wa (TAHOSSA) Tanzania heads of secondary schools associations wa mkoa wa Arusha katika ukumbi wa Karatu secondary.  Amesema Tahossa inatakiwa kusimama vizuri katika ngazi ya wilaya kwa sababu vikao vinavyofanyika Mkoani vya Tahossa, watekelezaji wake wakuu wapo katika ngazi ya wilaya. Vikao vya aini hii vikiwepo kwenye wilaya itasaidia kuimarisha vikao vya mkoa. Tunahitaji kuona mkoa wetu ukiendelea kupiga hatua katika kuongeza ufaulu wa wanafunzi kitaaluma.

Mh. Abbas Kayanda katika matukio tofauti wakati akihutubia walimu kwenye kikao cha wakuu wa shule Mkoa wa Arusha

Ameongeza kusema  umoja wa walimu wakuu wa sekondari Tahossa ni daraja linalowakutanisha na viongozi wa serikali. Lazima tuongezee idadi ya washiriki katika mikutano ya Tahossa katika ngazi ya wilaya ili kuibua maoni na changamoto ambazo zitaletwa ngazi ya mkoa na kufikishwa serikalini.

Mh. Kayanda amechukua nafasi hiyo kuwapongeza walimu wakuu kwa matokeo mazuri waliyoyapata kitaaluma katika mkoa wa Arusha. Amesema kwa ujumla tufanya vizuri kitaaluma lakini tukifanya tathimini ya wilaya moja moja na shule moja moja bado hali si nzuri. Amesema jukwaa hilo litumike kupeana maarifa ili kupata namna nzuri ya kuongeza kiwango cha ufaulu. Mkoa wa Arusha umeshika nafasi ya kwanza kwa ufaulu mzuri wa kitaaluma lazima tuje na mkakati wa kutunza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi katika shule zetu.

Wakuu wa shule wakimsikiliza Mh. Abbas Kayanda wakati wa hotuba ya ufunguzi

Akizungumzia kuhusu nidhamu Mh. Kayanda amesema lazima walimu tuendelee kuchukua hatua za kusimamia nidhamu kwa wanafunzi, swala la nizamu haliishii kwa wa wanafunzi peke yao. Amesema mwalimu lazima avae mavazi yenye staha, mwalimu mkuu lazima awe na fikra pevu katika utendaji wa kazi. Ameasa walimu katika vikao vya ndani vya shule kuacha kuoneana aibu kwenye utendaji usioridhisha na badala yake kujikita katika kujenga msingi mizuri ya kiutendaji. Amesema mtumishi yeyote anapaswa kuwa na nidhamu katika maisha binafsi na anapaswa kuwa nidhamu katika sehemu ya kazi.

Ameongeza kusema Mwalimu Mkuu hapaswi kuwa kiongozi wa kuwagawa walimu, Mwalimu Mkuu anatakiwa kujenga jumuiya yenye umoja sehemu ya kazi. Mwalimu mkuu ni kiongozi anayepaswa kulea badala kutenga watu, walimu tupendane katika misingi ya kazi. Walimu tunapaswa kusaidiana wenyewe kwa wenyewe, hatupaswi kuoneana wivu wa maisha, amesema maisha ni mipango. Walimu tunapaswa kushirikiana katika hali zote ili mwisho wa siku tuwe na mafanikio yenye kulingana.

Akizungumzia kuhusu kuongeza kiwango cha ufaulu, Mh. Kayanda amesema katika kuinua ufaulu kuna mbinu nyingi za kufanya ili kuongeza ufaulu. Amesema mkoa wa Arusha una utaratibu wakufanya mtihani wa pamoja wa kimkoa amesema ni vyema  kutengeneza utaratibu wa kufanya mitihani ya pamoja katika ngazi ya wilaya. Amesema  ni wakati sasa wakuja na mkakati wa kutokomeza  divison zero.

Akitoa salamu za shukrani Mwalimu mkuu John  Silvan Massawe  wa shule ya sekondari ya Mwandet wilaya ya Arusha, amesema wanapambana usiku na mchana kuendelea kuilinda nafasi ya kwanza kitaaluma waliyoipata. Amesema kikao cha Tahossa kimelenga kuandaa mikakati mipya ya kuinua ufaulu wa kitaaluma. Amesema wanafahamu fika kitendo cha Mkoa wa Arusha kuwa wa kwanza kwa ufaulu kitaaluma kuna watu watataka kutupita, amesema wanajipanga vizuri kuilinda nafasi yao.

wakuu wa shule Mkoa wa Arusha katika matukio fofauti wakati wa kikao

Akizungumzia kuhusu nidhamu Mwl Massawe amesema kuna shida ya malezi kwa vijana wa kizazi cha sasa, amesema kwa sababu walimu wakuu ni walezi wataendelea kuwaelekeza walimu namna nzuri za kutekeleza majukumu yao wakiwa katika maeneo ya kazi. Ameomba vyuo vya ualimu kuhimiza  misingi ya maadili ya ualimu katika Vyuo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa