• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

TAKUKURU YAZIDI KUBANA WATENDAJI WABADHILIFU

Posted on: October 27th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa wilayani Karatu imeokoa kiasi  cha million 56.7 zilizokuwa zimefanyiwa ubadhilifu. Fedha hizo zinajumuisha makundi mbalimbali ikiwemo mapato ya serikali, vyama vya ushirika, SACCOS na watu binafasi.

Akizungumza wakati wa urejeshwaji wa fedha hizo Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda amesema serikali ya awamu ya tano ikiongozwa na Mh. Dkt John Pombe Magufuli tangu imeingia madarakani imejikita katika kupambana na rushwa. Serikali inasimamia haki ndio maana fedha hizi zinarejeshwa, Mh. Kayanda amewapongeza Takukuru kwa kazi nzuri waliyofanya.

 Akizungumzia fedha za vitambulisho vya wamachinga zilizorejeshwa Mh. Kayanda amewaasa watumishi wa serikali na hasa watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanasimamia majukumu yao kwa uaminifu bila kufanya ubadhilifu.  Kiasi cha million 19.5 za vitambulisho vya wamachinga vya awamu ya kwanza ambazo zilikuwa zimepotea zimepatikana baada ya Takukuru kufanyia kazi taarifa ubadhilifu wa fedha hizo. Mh. Kayanda amesema vitendo vya namna hiyo ni vitendo ambavyo havifai na nivitendo ambavyo vinaweza kumfanya mtumishi afukuzwe kazi.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda (kulia) akikabidhi fedha za ofis ya kijiji zilizookolewa na Takukuru kwa Katibu tawala wa wilaya ya Karatu Bi, Faraja Msigwa

Mh. Kayanda ametoa rai pia  kwa watendaji vijiji kuheshimu fedha ambazo serikali inaleta kwa ajili ya miradi ya maendeleo. Lakini kuheshimu fedha ambazo wananchi wanachangia kwa ajili  ya miradi ya maendeleo, fedha hizo lazima zitumike kwa kufuata utaratibu wa serikali.  Amesema vitendo vya ubadhilifu wa fedha vikiachwa vikaendelea vitakuwa vinawavunja wananchi moyo katika kuchangia miradi ya maendeleo. Kiasi cha 2241,000 zimerejeshwa ambazo zilikuwa  za ujenzi wa ofisi kijiji lakini pia kiasi cha 623,000 zimerejeshwa kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ya Eyasi ambayo nazo zilifanyiwa ubadhilifu na uongozi wa kijiji.

Katika ushirika amesema serikali imedhamiria kuimarishwa ushirika lakini katika vyama vya ushirika vya wakulima wadogo wadogo SACCOS viongozi wao wamekuwa wakishirki kuhujumu vyama hivyo. Ametoa wito kwa viongozi wa vyama hivyo kujirekebsha nakuacha tabia za namna hiyo. Fedha ambazo wanachama wamechangia inapotakiwa kutumiwa lazima taratibu zifuatwe. Kiasi cha million 32, 793,847 ambazo kiasi cha 17,766,647 ilikabidhiwa saccos ya Mangola na 13,771,180 zimerejeswa mbulumbulu saccos  baada ya wanachama na viongozi kujikopesha bila kurejesha kwa mujibu wa taratibu zilizowekewa. Fedha nyingine zilizorejeshwa ni fedha za AMCOS ya Gilala kiasi cha 125,6000 fedha ambazo wanachama na viongozi walijikopesha bila kufuata utaratibu jambo lilowanyima wanachama wengine nafasi ya kukopa.

Matukio mbalimbali katika picha Mh. Abbas Kayanda akikabidhi fedha zilizorejeshwa na Takukuru

Kuhusu swala la mikataba ya ajira Mh. Kayanda amesema  katika kuajiri huwa kunakuwa na ajira za muda mrefu na ajira za muda mfupi. Ametoa rai kwa waajiri wote wa makapuni binafsi kuhakikisha wanatoa mikataba kwa watumishi wao. Mh. Kayanda amezungumzia hilo baada ya watumishi wa Usafi Group waliokuwa wanamdai muajiri wao kiasi cha 6000,00 kupewa fedha zao baada ya muajiri wa kampuni hiyo kuwaachisha kazi bila kuwalipa mishahara ya miezi miwili. Kiasi hicho cha fedha kimepatikana baada ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kufuatilia swala lao kwa muajiri wa Usafi Group.

Mh. Kayanda amesema watu wa Takukuru wataendelea kukagua miradi mbalimbali ya mendeleo ili kujiridhisha kama miradi inayojengwa inaendana na thamani fedha zilizotolewa. Ametoa rai kwa wananchi kutoa taarifa zozote zinazohusiana na rushwa katika ofisi ya Takukuru ili hatua stahiki zichukuliwe haraka ili watu wapate huduma bila usumbufu. Hii itasaidia  kuhakikisha mazingira yote ya utoaji wa  rushwa yanadhibitiwa.

Kamanda wa Takukuru wilaya ya Karatu Bi, Atuganile Stephen amesema hakuna mtu aliye juu ya sheria, kama mwananchi anaona amedhulumiwa au kunyanyaswa katika kutafuta haki zake ni vyema akatoa taarifa Takukuru. Lakini pia kamanda wa Takukuru ameshukuru kwa ushirikiano wanaoupata kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya, ushirikiano ambao umesaidia kubaini mianya mingi ya ubadhilifu kwenye miradi ya maendeleo.

Nao wananchi waliorejeshewa Ndg. Paskali Safari na Samweli Bura wameishukuru serikali na Takukuru kwa kuwasaidia kurejesha fedha zao na kusimama pamoja nao katika  kipindi cha kudai haki zao. Wametoa rai kwa wananchi wanapopata shida kama walizopata wao wasisite kutoa taarifa Takukuru au ofisi ya Mkuu wa wilaya.

Wananchi wanapaswa kukimbilia serikalini kupata msaada, wamesema wamefarijika kuona serikali imewasaidia kupata fedha zao bila kudai kiasi chochote cha fedha. Amesema jambo hilo limezidi kuwajengea imani  na Taasisi ya Takukuru na serikali kwa ujumla.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa