• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

“TANESCO, TUFANYE KAZI” TUMALIZE MALALAMIKO

Posted on: April 9th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Utoaji wa huduma kwa wateja lazima uimarike hasa kwenye huduma za dharura ambazo zinahitaji utatuzi wa haraka. Ili kujenga imani kwa wananchi kwamba mnajali na kusikiliza shida zao kwa wakati hasa wakati changamoto zinapojitokeza. Tujiwekee utaratibu  mzuri wa kutoa taarifa kwa wananchi hasa zinazohusu marekebisho ya umeme ili kuwe na uelewa wa pamoja katika kutoa huduma.

Tukijenga mawasiliano mazuri kati ya shirika la umeme na wateja itahamasisha watu wengi kujitokeza kupata huduma. Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokuwa akizungumza na wafanyakazi wa shirika la umeme Tanesco Karatu. Amesema shirika la umeme linafanya kazi nzuri  sana hasa kipindi hiki cha masika chenye changamoto nyingi ya miundo mbinu ya umeme kupata hitilafu. Lakini pia changamoto ya matope kwenye barabara ili kufikia sehemu zenye shida imekuwa ikiathiri utendaji kazi.

Mh. Abbas Kayanda akiwa na meneja wa Tanesco Karatu baada ya kikao kifupi na wafanyakazi wa shirika hilo.

Mh. Kayanda amesema katika kuimarisha mawasiliano watendaji wa shirika la umeme  lazima wakubali mabadiliko na waongeze kasi ya kufanya matengenezo pindi taarifa za hitilafu ya miundo mbinu zinapotolewa. Kuna changamoto za nyaya kukatika au nguzo kuanguka, shida zinazoweza kusababisha hatari ya kupoteza maisha kwa mwanadamu. Taarifa kama hizi zikitolewa na wananchi watendaji wa Tanesco msijivute kushughulikia, kwa sababu inatoa picha mbaya kwa wananchi. Dhamira yetu ijikite katika kutatua kero, ameongeza kusema nafahamu watumishi wa shirika la umeme Tanesco ni wachache lakini tujigawe kwa uchache wetu ili wananchi wapate huduma.

Mh. Kayanda amesema kumekuwa na malalamiko mengi kwa wananchi juu ya utendaji kazi wa shirika la umeme hasa katika utoaji wa huduma. Malalamiko hayo hayaleti afya katika kuendesha shirika, na badala yake yanajenga taswira mbaya. Amemuelekeza meneja wa shirika la umeme Karatu; kuja na mkakati  madhubuti, utakaowezesha njia bora za kutatua kero za wananchi kwa wakati. kwa  kuanza kuainisha mafundi  wa umeme ambao, kama mwananchi anataka huduma ya kusuka waya katika nyumba yake  wanaweza kufanya  kazi kwa weledi wa taaluma.

Mh. Kayanda ameongeza kusema kuwe na uwazi ili kama mteja au mwananchi anahitaji kumuona meneja wa Tanesco aweze kumpata. Badala ya utaratibu wa sasa ambao mwananchi akitaka kumuona meneja anazungushwa bila ya kuwa na sababu za msingi. Tukiboresha utoaji wa huduma shirika litaongeza wateja wapya wengi wanaohitaji kuunganishwa na huduma ya umeme. Kwasababu wananchi watafahamu hatua za kufuata ili kuunganishwa na huduma ya nishati ya umeme. Amesema kuacha wananchi hewani bila kuwaeleza mahitaji yanayohitajika kwa mteja ili aweze kuunganishwa na umeme kunasababisha wananchi kuona wanapuuzwa tujifunze customer care.

wafanyakazi wa shirika la tanesco wakiwa katika kikao wa mkuu wa wilaya ya karatu ambaye hayupo pichani

Naye Meneja wa umeme wilaya ya Karatu Mhandisi Wilhelm Chami amemshukuru mkuu wa wilaya ya Karatu kwa kutembelea na kujionea utendaji kazi wa shirika hilo. Ameahidi kufanya mageuzi makubwa ya kiutendaji kwa kuhakikisha wanajenga mazingira ya uwazi katika utendaji wa kazi. Katika taarifa yake amesema shirika la umeme Karatu linasema kuna idadi ya watu zaidi  ya 3000 wanaojiunga kupata huduma ya umeme kwa mwaka na kwa  sasa kuna waatu zaidi ya 15000 ambao tayari wameshaunganishwa na umeme ukilinganisha  na wilaya nyingine.

Katika unganisha umeme vijijini (Umeme wa Rea) Mhandisi Ndg Chami amesema kuna kampuni mpya ya Etdco ambayo ni kampuni tanzu ya Tanesco  imepewa kazi ya kusambaza umeme vijijni. Kwa sasa Project manager wa kampuni amesha ripoti na ameenda  Dar es salamu kukusanya vifaa kwa ajili kuanza kufanya kazi ya kusambaza umeme vijijni.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa