• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

TUMEWEKEZA KATIKA UJENZI WA MIUNDO MBINU YA ELIMU

Posted on: March 29th, 2019

Madiwani wa wilaya ya Karatu pamoja na watendaji mbalimbali wa Halmashauri wametembelea leo shule ya OLdean seondari, shule ya Msingi Gyetighi na Kituo cha watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu. Ziara ililenga kuona shughuli zinazofanywa na shirika la Rift Valley Children Fund ambalo linashirikiana na serikali kuimarisha miundo mbinu ya elimu.

Mkurugenzi wa Rifty Valley Ndugu Mmassy amesema katika kipindi cha miaka 15 wametoa vijana waliohitimu elimu ya juu 79 katika fani mbalimbali na kuajiriwa. Amesema pamoja na mafanikio hayo shirika limeendelea kuhakikisha wanafunzi wanapata elimu bora. Shirika  limejenga Maktaba pamoja na Kuweka vitabu, Maabara na vifaa vyake, Jengo la utawala, Madarasa,  pamoja na nyumba za walimu.

Ndugu Mmassy amesema wao wanajihusisha pia na kulea watoto wanao toka katika mazingira magumu na yatima. Shirika limeajiri wakinamama zaidi 130 kwa ajili ya kulea watoto kwenye kituo chao. Ndugu Mmasy amesema wanatoa huduma za afya kwa wananchi wa Oldean na kutoa rufaa pia kwenda Hospitali ya Fame na Selian  Jijini Arusha. Wanatoa pia mikopo kwa wananchi wa eneo la Oldean ili kuwainua kiuchumi.

Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari  Oldean ndugu  Yuda John ambaye shule yake ilitembelewa, amesema shule ina walimu 15 wenye ajira ya kudumu na walimu wa muda 11. Shirika linasaidia watoto 46 ambao ni watoto yatima na kusaidia kulipa mishahara ya walimu wa muda. Mwalimu Yuda  amesema shirika la Rifty Valley Children Fund, linampango wa kujenga mabweni kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka mbali na yatachukua wanafunzi 480.

 Mwalimu Yuda  amesema lengo ni kuongeza uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi kama ilani ya chama cha mapinduzi inayosimamiwa na serikali ya awamu ya tano inavyoelekeza. Elimu ya msingi na sekondari mpaka kidato cha nne ni bure, ili kuruhusu  watoto wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali kupata elimu. Amesema changamoto inayowakabili  kwa sasa ni upatikanaji wa nishati ya umeme, amemuomba katibu Tarafa wa tarafa wa Karatu kuwasaidia kupata umeme kupitia mpango wa REA.

Madiwani pia walipata nafasi ya kutembelea shule ya msingi Gyetighi ambayo inasimamiwa na serikali ikishirikiana na Rift Valley Children Fund. Mwalimu mkuu ndugu Fidelis,Anthony amesema shule ina walimu 8 wa kuajiriwa na serikali na walimu 16 wa muda na walimu wanafunzi 5. Mwalimu Fidelis amesema shirika linatoa chai kwa walimu asubuhi na uji kwa wanafunzi, chakula cha mchana kwa wanafunzi na walimu pamoja na kutoa huduma ya afya.

Shirika linatoa elimu ya malezi kwa walimu hasa ukizingatia kwamba shule yao ni ya mfano, mwanafunzi hachapwi bali anapewa adhabu ndogondogo kama kupiga magoti, kuruka kichura chura na kushauriwa. Shirika limejenga viwanja vya michezo pamoja na kutoa vifaa vya michezo na kuweka uzio na mageti. Shirika linatoa motisha kwa walimu ili kuwapa ari ya kufanya vizuri katika ufundishaji..

Mweneyekiti wa Halmashauri Mhe. Jublate Mnyenye ameshukuru kwa namna ambavyo Shirika linavyofanya kazi kwa niaba ya serikali. Ameomba watumishi wafanye kazi pamoja na shirika hilo na kutoa ushirikiano. Amesema madarasa hayawezi kufaulisha wala maabara peke yake; kwa kuwaachia majukumu walimu peke yao, wazazi timizeni wajibu wa kuwasimamia watoto ili wafaulu vizuri. Mhe. Jublate amesema kama kunajambo linaleta kikwazo katika maswala ya utendaji, litolewe taarifa sehemu husika hatua kwa hatua. Amesema tukipuuzia  jambo likawa kubwa  likaenda ngazi za juu bila kufuata hatua litaonekana kuna Personal interest.  

Mhe. sabina na wataalamu wakiangalia kwa tumiaa kifaa maalumu  kuangalia sampuli ya jani katika maabara ya bailojia 

 Waheshimiwa madiwani wakisikiliza kwa makini maelekezo ya mkuu wa shule Ndugu Yuda John kwenye maabara ya Kemia

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa