• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

“TUPANDE MITI, KARATU IWE YA KIJANI”

Posted on: April 19th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Miti milioni moja na nusu inatarajiwa kupandwa katika wilaya ya Karatu, miti hiyo itapandwa katika taasisi za serikali na watu binafsi lengo likiwa ni kufanya wilaya ya Karatu kuwa ya kijani. Wito umetolewa kwa wananchi kushiriki katika zoezi la upandaji wa miti kwa kuhakikisha kila familia inapanda miti kumi katika eneo inaloishi.

Hayo yamesemwa na Katibu tawala wa wilaya ya Karatu Bi. Faraja Msigwa alipoongozwa wananchi na watendaji wa serikali katika siku ya kupanda miti akimuwakilisha Mkuu wa wilaya ya Karatu. Zoezi la upandaji wa miti limefanyika katika eneo inapojengwa  hospitali ya wilaya ya Karatu katika kijiji cha changarawe. Amesema lazima tupande miti ili kuzuia mmonyoko wa udongo unaosababishwa na ardhi kuwa wazi. Amesema kupanda miti kuna faida kubwa, kwanza inasaidia kutunza na kuweka hali ya hewa vizuri na kupata miti ya kivuli  inayosaidia kupata maeneo ya kupumzika.

Wananchi wakishiki zoezi la upandaji miti katika Hospital ya wilaya ya Karatu.

Bi, Msigwa amesema zoezi la kupanda miti ni zoezi endelevu tunahitaji kutunza vyanzo vyetu vya maji, ametoa rai kwa watendaji wa serikali  kuhamasisha watu katika maeneo yao ya kiutendaji ili kuhakikisha mikakati iliyowekwa na wilaya inafikiwa. Bi Msigwa amepongeza na kushukuru wadau mbalimbali walioshirikiana na wilaya katika  kuwezesha zoezi la kupanda miti linafanikiwa.

Afisa misitu wa wilaya Ndg. Regnald Hallu amesema wadau wamazingira wameweza kupanda miti akatika kijiji cha Ayalalio, Buger, kitongoji cha Ngorong’aida na maeneo ya taasisi kama Qaru sekondari, Oborshan sekondari, Endabash sekondari Endarofta sekondari, kitongoji cha bwawani na bado zoezi la usambazaji wa miche ya miti inaendelea.

Ndg. Hallu amesema taasisi ya Mviwata ya Arusha imeweza kuanzisha mradi wa vitalu vya miche ya miti katika vijiji vya Slahamo,  Buger, Rhotia Kainam, Kambi ya simba na Upper kitete. Amesema jumla ya miti 15000 imepandwa katika msitu wa Kansay. Amessema taasisi ya Mviwata imefanikiwa kufikia vijiji 20 na kufanikiwa kupanda miti zaidi ya 63000.

Naye Makamu mwenyekiti wa Mviwata Bi. Anna Efata ametoa shukrani kwa Halmashauri Karatu kwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na Mviwata Arusha. Amesema sasa ni jukumu la wananchi kutunza na kuhifadhi miche ya miti iliyopandwa, haipendezi kuona watu wanafanya uharibifu katika maeneo ambayo miche ya miti imepandwa. Swala la kulinda na kuhifadhi miche ya miti ni jukumu letu sote.

Bi. Efata ameshukuru wadau wengine kama Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, wadau wa IDP kupitia mradi wa kilimo endelevu , wadau wa shirika la World vision na Ganako youth foundation. Amesema maono ya Mviwata ni kuendelea kuhamasisha na kushauri wananchi watunze mazingira.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Karatu Ndg. Ally  Mdangaya akipanda mti wakati wa zoezi la upandaji wa miti.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa