• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UANDIKISHAJI WATOTO, DARASA LA KWANZA WAFIKIA 93%

Posted on: February 6th, 2020

Kikao cha baraza la madiwani cha robo ya pili ya mwaka kimekaa siku ya kwanza, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Karatu. Madiwani wa kata zote wamewasilisha taarifa za kata kwenye kikao cha baraza.

Katibu wa kikao cha baraza la Madiwani Ndugu Waziri Mourice amesema tangu serikali ya awamu ya tano imeingia kumekuwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi. Amesema kuna wanafunzi 4084 wa sekondari walioripotiwa kufaulu; lakini walioripoti shuleni mpaka sasa ni wanafunzi 3574, kuna wanafunzi 510 ambao hawajaripoti shuleni. Hawa wanafunzi wapo kati kata zetu, amesema wanafunzi ambao hawahudhurii shuleni kwa upande wa kata za Baray na Mang’ola huwa wanaenda kufanya kazi katika mashamba ya vitunguu.

 Amesema uandikishaji wanafunzi wa awali ni 73% katika malengo ya uandikishaji wa 100%, uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza ni 93 % kuna 7% ambao bado hawajaandikishwa. Ndugu Mourice amesema waheshimiwa madiwani ni wenyeviti wa kamati za maendeleo katika kata. Ameomba wadiwani kuhakikisha wanafunzi ambao hawajaripoti shuleni na wanapaswa kuandikishwa mashuleni wanawafuatilia ili wanafunzi hao waandikishwe.

Ndugu Mourice amesema ili kuongeza kiwango cha ufaulu kitaaluma kwa wanafunzi, ni vyema wazazi kuwachangia chakula  wanafunzi. Kuna kamati za chakula za wazazi  ambazo ndizo zinaweka utaratibu wa kuchangia chakula. swala la uchangiaji wa chakula haliwahusu walimu, ameomba waheshimiwa madiwani kufanya ufuatiliaji wa michango hiyo ili wanafunzi waweze kupata chakula wanapokuwa shuleni.

wanafunzi wa shule ya Msingi wilayani Karatu, katika moja ya Maadhimisho yao wakiomba Wazazi na Walezi kujali haki zao.

Diwani wa kata ya Daa Mhe. Benedicto Modaha amesema bado kuna changamoto za wazazi  kupuuza kuchangia chakula shuleni, ili watoto wapate chakula mchana. Amesema upo umuhimu wa watendaji wa serikali kushirikiana na viongozi wa serikali katika kata, ili wazazi wahamasishwe kuchangia vyakula shuleni. Amesema awali walimu wakuu katika kata ya Daa walikuwa wanapingana na watendaji wa kijiji jambo ambalo liliyumbisha ufanisi wa kukusanya michango hiyo. Mhe. Modaha amesema wapo wazazi walikuwa wanakataa kuchangia na hivyo kusababisha watendaji wa vijiji kuingia kwenye gharama za kuendesha kesi. Amesema bado upo umuhimu wa kuendelea kuwapa elimu zaidi na kuhimiza wazazi  kuchangia chakula kwa ajili ya watoto, ili watoto waweze kuzingatia masomo vizuri.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa