• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UFUGAJI WAINUA KIPATO CHA WANANCHI

Posted on: May 25th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Familia zenye maisha duni zimeongeza kipato baada ya shirika lisilo la serikali  la Food for his children kujenga uwezo kwa wananchi kupitia miradi ya ufugaji na kilimo. Ahueni hiyo ya maisha imesaidia familia duni kujiongezea kipato kwa kupata fedha kwa mahitaji ya wanafunzi na uwezo wa kujenga na kuwekeza katika shughuli mbalimbali za uzalishaji.

Elimu waliopata wananchi ya ujasiramali na kujengewa uwezo wa kufuga mifugo kwa njia za kisasa isambae kwa wananchi wengine. Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea miradi mbalimbali inayoendeshwa na shirika la food for his chidren katika kijiji cha G-lambo. Amesema Food for his children wanafanya kazi nzuri na wanasaidia  serikali katika kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi. Ufagaji wa kisasa unaondoa adhaa ya mfugaji kupoteza muda mwingi wa kuswaga mifugo kutafuta malisho, badalayake anaweza kufuga kwa kwa kuhifadhi kwenye banda na kutumia majani  na mabaki ya majani ya mazao kulisha mifugo.

Mh. Abbas Kayanda akikagua miti ya matunda katika shamba la mkulima katika kijiji cha G-lambo

Amehimiza kuweka mkazo katika kilimo cha kisasa amesema wataalamu wa kilimo wanapaswa kuwasaidia wakulima katika kutambua mbegu bora za mazao. Amesema mikakati hiyo itawezekana kama wataalamu watatoa elimu na kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa wakulima.  Katika ziara hiyo Mh. Kayanda aliweza kujionea uwezeshaji na uhamasishaji uliofanywa na shirika la food for his children kwa wananchi katika kujihusisha na kilimo cha bustani za mboga katika makazi yao.

Akizungumza kuhusu namna miradi inavyotekelezwa Mkurugenzi wa shirika hilo Bi, Honorina Honorat amesema wanaweka mkazo katika miradi kwa kuhimiza wakulima kuwa na banda la zuri la mifugo. Amesema shirika lilileta mbuzi wa kisasa aina ya sane ambao waliweka utaratibu mzuri wa miradi hiyo kupokelewa na wananchi na kuingia katika umiliki wao. Jambo ambalo limeongeza ari kwa wananchi kujihusisha na ufugaji wa kisasa.

Amesema wananchi wananufaika na ufugaji kwa sababu walikubali kutumia mbinu bora za ufugaji kufuata kanuni za kilimo ikiwa ni pamoja na kuchagua mbegu bora za kupanda na kujihusisha katika upandaji wa miti ya matunda. Sambamba na shughuli hizo shirika limewezesha wananchi kupata elimu ya awali ya usimamizi wa fedha. Bi, Honorati amesema shirika linaweka msisitizo kwa wananchi kujenga vyoo bora ikiwa ni mkakati wa kuboresha mazingira ya kuishi, na kutengeneza vichanja kila nyumba kwa ajili ya kuhifadhi vyombo.


Mh. Kayanda akiwa katika banda la mbuzi la Bi, Fausta Anton

Wakizungumza kuhusu namna walivyonufaika na miradi Bi. Elizabeth Katarina amesema mradi wa kufuga mbuzi umemuwezesha kupata maziwa lita moja au zaidi kwa kila mbuzi wa maziwa na kiwango hicho hutegemea na namna anavyowalisha. Amesema pamoja na kupata maziwa ameweza kumalizia ujenzi wa nyumba ambao awali alikuwa ameshindwa. Hali ya maisha imebadilika ameweza kuongeza idadi ya mbuzi na kujenga banda zuri  la mbuzi na la kisasa.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa