• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UHAKIKI WA MIPAKA YA HIFADHI, WANANCHI MSIWE NA WASIWASI

Posted on: June 20th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Zoezi la kuhakiki mipaka ya hifadhi ya ziwa Manyara na kijiji cha Buger ni maelekezo ya serikali yaliyofikiwa baada ya kikao kilichohusisha mawaziri tisa kutoa mapendekezo. Uhakiki utakuwa shirikishiki kwa kuhusisha wawakilishi wa wananchi wa kawaida, wawakilishi wa serikali ya kijiji, wataalamu wa Halmashauri, wataalamu wa tume ya mipango bora ya ardhi na kutakuwa na wawakilishi wahifadhi wa ziwa Manyara na  uhakiki utafanyika kwa kutumia tangazo la gazeti la serikali na kwa kutumia vipimo vya technolojia ya kisasa GPS.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda kabla ya taarifa za uteuzi, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Ayalaliyo. Amesema zoezi la uhakiki wa mipaka litahusisha kijiji cha Endonyawet baada ya kumaliza kuhakiki katika kijiji cha Buger na maeneo yaliyowekewa kipaombele katika kijiji hicho kama kitongoji cha Gahabiye, Ayabea Ants-Gamdi na Ayalabe. Amesema zoezi la kuhakiki mipaka ya hifadhi ya ziwa manyara halihusiani kuondoa watu. Amesema wananchi hawapaswi kutaharuki juu ya zoezi hilo, baada ya kuhakiki taarifa itapelekwa serikalini, kama kutakuwa na jambo jingine serikali itatoa taarifa. Amesema uhakiki huo utasaidia kujua mipaka halisi ya eneo la ardhi ya hifadhi ya ziwa Manyara. Amesema kwa sasa kuna mipaka ya mawe matatu jambo ambalo linaleta mkanganyiko kwa wananchi kufahamu mpaka halisi wa hifadhi.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na viongozi wa kata ya buger katika mkutano wa hadhara

Mh. Kayanda amesema wananchi wa Buger wanapaswa kujenga uhusiano mwema na hifadhi ya ziwa Manyara badala ya kujenga mahusiano ya kuvutana. Wananchi wa Buger mnapaswa mumsumbue diwani wenu kuhusu ujenzi wa miradi ya maendeleo. Maendeleo hayawezi kupelekwa sehemu ambayo kila siku watu wanazozana; ameongeza kusema  mwaka ujao wa fedha  kata ya Buger kuna ujenzi wa kituo cha afya chenye thamani ya million 400 kwa fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri, wananchi wanapaswa kujadili na kuweka mkakati juu ya ujenzi  wa kituo hicho cha afya.

Amesema ujenzi wa kituo cha afya utasaidia wananchi wa Buger kutotembea umbali mrefu kufuata huduma za afya katika kata ya Endabash. Amesema kata ya Buger imekuwa nyuma kimaendeleo kwa sababu ya migogoro na hilo sio jambo jema. Ni wakati sasa wa kumuunga mkono diwani wenu ili kuchochea maendeleo katika kata ya Buger.

Diwani wa kata ya Buger Mh. Bsili Gitilo akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara

Naye mwenyekiti wa Halmashauri Mh. John Lucian amesema ili kujenga mawasiliano mazuri na Hifadhi ya ziwa Manyara, ataweka utaratibu wa kuwa na muwakilishi wa Tanapa katika vikao vya baraza la madiwani. Hiyo itasaidia kuimarisha mawasiliano ya moja kwa moja kati hifadhi ya ziwa Manyara na wananchi.

Amesema katika kuleta uelewa wa pamoja elimu zaidi ya ujirani mwema inahitajika kwa wananchi, serikali za Halmashauri za vijiji zitoe mwaliko katika mkutano mkuu wa Halmashauri ya kijiji kwa  Tanapa ili kuja kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwa na mahusiano mema na kuzidi  kushirikiana. Jitihada hizo za kuelimisha kuhusu ujirani mwema ziende katika vikao vya maendeleo vya kata ili kujenga jamii yenye muitikio chanya juu ya maeneo yaliyotengwa na serikali kwa ajili ya hifadhi.

wananchi wa kata ya Buger wakiwa katika mkutano wa hadhara ofisi ya mtendaji kata

Katika mkutano huo diwani wa Buger Mh. Basili Gitilo amesema mahusiano mabaya katika ya wananchi na  hifadhi ya ziwa Manyara imesababisha kasi ya maendeleo katika kata ya Buger kufifia. Amesema  ni vyema wananchi kufuata utaratibu na kuelewa sheria za hifadhi ili kujiepusha na  vitendo visivyofaa vinavyofanywa na watu wachache ambavyo vinaharibu mahusiano ya jamii nzima ya watu wanaoishi katika kata ya Buger. Amesema kulikuwa na ujenzi wa soko la wanawake ambalo lilipaswa kujengwa na hifadhi ya ziwa Manyara katika kijiji cha Buger lakini kutokana kuvutana vutana na hifadhi soko hilo halijajengwa mpaka sasa.

Mhifadhi Mkuu wa Tanapa Bi, Noelia Myonga akizungumza wakati wa kikao

Mhifadhi Mkuu wa Tanapa Bi, Noelia Myonga amesema katika maisha huwezi kuchagua jirani, amesema ni vigumu sana watu wanaovutana mara kwa mara kukaa na kuzungumza mambo ya maendeleo. Amesema katika kujenga soko la wanawake mradi ulikwama kwa sababu wananchi walishindwa kuweka 30%  ya kuchangia soko hilo, hivyo mamlaka kushindwa kuanza kutekeleza mradi, hata hivyo mradi huo bado utafanyiwa kazi. amesema andiko linafanyiwa mapitio na mhandisi wa Halmashauri ili kujua kwa sasa soko hilo linaweza kujengwa kwa kiasi gani cha fedha.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa