• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UHALIFU MATALA, SASA BASI

Posted on: January 25th, 2020

Mkuu wa wilaya ya karatu Mhe. Theresia Mahongo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Matala. Mkutano huo ulilenga kubaini watu wanaojihusisha na uhalifu katika maeneo ya Matala, Yaeda ya chini  na kuhatarisha amani na usalama kwa wananchi.

Mhe. Theresia Mahongo amesema hatakubali mambo ya uhalifu yatokee kwenye eneo lake, amesema wahalifu wengi wapo katika kijiji cha Matala.  Mhe. Mahongo amewapongeza wananchi wanaoendelea kutoa ushirikiano kwa serikali dhidi ya uhalifu unaofanyika, amesema Mhalifu mmoja alikamatwa katika kijiji cha Yaeda ya chini lakini pia msako umeendelea kimya kimya na katika msako huo ng’ombe mmoja ambaye alikuwa ameibwa alikamatwa mnada wa Meatu.

Mhe.Mahongo amesema ameambiwa kwamba wahalifu wamekuwa wakisaidiwa na baadhi ya wananchi na watendaji wa serikali. Ameomba wananchi kuwakataa watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu kama ukoma. Mhe. Mahongo amewaongoza wananchi kupiga kura za siri ili kubaini na kujiridhisha  kwa kupata majina ya watu wanaojihusisha na shughuli za uhalifu. Mhe. Mahongo amewaambia hata alipofika kwenye kijiji amekuta kuna mwananchi amejeruhiwa na mwanachi mwenzake vibaya sana. Amesema lazima hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake, amesema Mtuhumiwa amekuwa na matatizo ya kuogofya katika kijiji cha Matala. Amesema anataka kumuona askari atakayemuachia huyo Mhalifu tena ili aendelee na shughuli za kuhatarisha amani na usalama katika kijiji cha Matala.

Mwananchi akipewa msaada wa kupiga kura ya siri kubaini watu wanaojihusisha na Uhalifu Matala.

Mhe. Mahongo amesema ameambiwa kuna watu wanavamia vibanda usiku na kubomoa ikiaminika wanakula wali, ndizi, wanakula maandazi. Amesema mtu anayefungua mlango wa mwenzake bila ufunguo ni mwizi, ameonya watu wanaofanya hivyo muarubaini wao unakuja. Amesema kuna Sungusungu katika kijiji cha Matala lakini Sungusungu ya Matala haifanyi vizuri. Amesema Sungusungu ni watu wanaofanya ulinzi shirikishi, amesema lazima Sungusungu wafuate sheria amehimiza wananchi kukaa na kupanga viwango vya faini. Amesema  kwa namana wanavyotoza fani kwa sasa laki tatu si sawa, Mhe Mahongo amesema Mkuu wa polisi atakwenda  kuwapa mafunzo Maalumu Sungusungu hao kijijini Matala ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi.

Mhe. Mahongo amewaelekekeza viongozi wa kijiji kujiandaa ili waweze kufanya zoezi la mgambo kwa vijana. Amesema kuna Mgambo anaitwa Lukasi amesema ameshamvua cheo cha Mgambo na wamemchukulia cheti chake, amesema kama Lukasi anakuja Matala akae kama Mwanachi wa kawaida na sio kama Mgambo. Amesema tuhuma Mbalimbali ndio zilizomvua cheo hicho huko Mang’ola ikiwa ni pamoja na rushwa.Amesema  Kuna kijana anaitwa Jafari  naye anashirikiana na Mkuu wa kituo cha Ibaga wilaya ya Mkalama kukamata wananchi bila utaratibu. Mhe. Mahongo amemuonya Mwanamgambo Jafari kuacha tabia hiyo  mara moja.

Mhe. Mahongo amesema swala la usalama ni kitu cha kwanza kuliko mambo mengine yote, ameomba wananchi kujitolea na kuanza kujenga kituo cha polisi kijiji cha Matala. Mhe. Mahongo ametoa Mifuko Ishirini kwa kuanzia, ili kuanza kujenga kituo cha polisi. Ameomba wananchi wamuunge mkono katika ujenzi wa kituo cha polisi Matala. Amesema kujenga kituo cha polisi kutawezesha askari kuwa na silaha, amesema kujenga kituo cha polisi ni muhimu kwa sababu askari watapata sehemu ya kuhifadhi silaha. Amesema kwa hali ilivyo kijiji cha Matala kinahitaji kuwa na kituo chenye Maaskari angalau wanne kwa kuanzia . Ameomba wananchi kuanza kutoa mchango wa shilingi elfu kumi, amemuelekeza Mtendaji wa kijiji kuandaa kibali cha kukusanya mchango na kukukipeleka  ofisi ya Mkuu wa wilaya na ameahidi kukipitisha kibali hicho,  kwa sababu kila mwananchi kwenye mkutano wa hadhara  amekubali kuanza ujenzi wa kituo cha Polisi.

Mwananchi akiwa anasaidiwa vyombo vya ulinzi katika zoezi la upigaji wa kura za siri

Awali ndugu Abbasi Kayanda  amesema kwenye Mkutano na wananchi wa kijiji cha Matala  kwamba kumekuwa na matatizo ya wizi wa mifugo. Amesema jambo hilo linakera, katika vijiji 57 vya wilaya ya Karatu kijiji cha Matala kimekuwa kikiripotiwa  matukio ya wizi mara kwa mara. Ndugu Kayanda amesema katika msako uliofanywa katika mnada katika Wilaya ya Meatu, ng’ombe walioibwa katika kijiji cha Yaeda chini wilaya ya Mbulu walipatikana mnada wa Meatu.

Ndugu Kayanda amesema pamoja na kufanya mkutano tunataka kufahamu tatizo liko wapi ?? Amesema hata kama kuna tatizo la wizi, mwizi hawezi kutoka mbali kama hakuna mwizi anayeshirikiana naye eneo la karibu. Amesema wananchi wamekuwa wakiona haya na kuwataja watu wanaojihusisha na shughuli za uhalifu katika kijiji cha Matala. Ndugu kayanda amesema mkutano huo unalenga kupata ufumbuzi wa matatizo ya uhalifu yanayofanyika katika kijiji cha Matala

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa