• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UHAMASISHAJI WA USAFI WA MAZINGIRA WAWEKEWA MKAZO

Posted on: June 4th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Wananchi wahamasishwa kujenga vyoo bora ili kuepuka magonjwa ya mlipuko yanayotokana na uchafu wa mazingira. Huku mkazo mkubwa ukiwekwa katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa vyoo bora, na matumizi sahihi ya vyoo. Ikiwa ni pamoja na kuhakikisha  hatua stahiki zinachukuliwa na viongozi katika kuhimiza wananchi kujenga vyoo bora.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati akifungua semina ya ukusanyaji wa takwimu za usafi wa Mazingira, iliyohudhuriwa na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji , na watendaji wa Kata katika ukumbi wa ofisi ya Afisa Tarafa Karatu. Ameongeza kusema hakuna mbadala wa afya ndio maana katika seikali za vijiji kuna kamati ya kudumu ya huduma za jamii ambayo ndani yake kuna maswala ya afya na moja ya jukumu lake ni kusimamia na kuhimiza usafi kwa wananchi.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya mazingira 

Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa takwimu sahihi za familia zenye vyoo bora, amesema wenyevitii wa vitongoji watakuwa wanawasilisha taarifa kila tarehe 25 ya kila mwisho wa mwezi kwa ofisi ya mtendaji wa kijiji ili aweze kuziandaa na kuwasilisha taarifa hizo kwa mtendaji wa kata. Amesema taarifa hizi za takwimu h zitakuwa zinakusanywa na kutolewa taarifa kwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri kabla ya ya tarehe 5 ya mwezi unaoanza. Amesema bado takwimu zinaonesha familia nyingi zina vyoo vya asili, amesema katika takwimu hizo ni kata ya Karatu pekee ndio ambayo haina takwimu za watu wasio na vyoo.

matukio katika picha wakati wa uzinduzi wa semina ya usafi wa mazingira kwa wenyeviti na watendaji wa vijiji na kata 

Amesema zoezi la ukusanyaji wa takwimu sahihi za vyoo litakuwa endelevu ili kuweza kupata tathimini ya wapi tumetoka ?? na tunaenda wapi, ametoa wito kwa viongozi wa Karatu kufanya zoezi hilo kwa ukamilifu wake, istokee watu wakatoa takwimu za kupika. Amesema anajua kazi kubwa wanazozifanya watendaji katika kusaidia usimamizi wa miradi ya maendeleo. Kampeni ya usafi wa mazingira iliyofanywa awali imeleta matokeo mazuri na lengo ni kujenga jamii yenye afya bora.

Amesema kuna kaya 219 kwa takwimu za sasa zisizo na vyoo, amesema katika uhamasishaji ulioofanywa tarehe 21, Desember 2018 kwa siku tisa jumla ya kaya 404 hazikuwa na vyoo. Mwaka 2019  kaya zikapungua na kufikia 155 ambazo hazikuwa na vyoo na mwaka 2020 kaya zikaongezeka na kufikia 274 ambazo hazikuwa na vyoo. Lazima tuendelee na msukumo wa kuhimiza wananchi kujenga vyoo bora. Ile kampeni tuliyoianza lazima tuiwekee mwendelezo mzuri wa ufuatiliaji.

Matukio katika picha wakati wa uzinduzi wa semina ya usafi wa Mazingira

Wananchi wanapaswa wajenge vyoo bora na sio bora vyoo, bado watendaji wanakazi kubwa sana ya kufanya katika kuboresha mazingira ya usafi. Majukumu ya viongozi ni pamoja na kutembelea taasisi zilizopo kwenye maeneo ya utawala kwa kufuatilia hali ya usafi wa mazingira ya taasisi hizo. Hakuna mbadala wa afya, lazima wananchi wawe na afya njema ili waweze kujikita katika shughuli za uzalishaji mali. Swala la afya linapaswa kuwa ajenda ya kudumu katika vikao vyetu.

Naye kaimu Mkurugenzi Ndg. Godfrey Luguma amesema katika kampeni ya usafi wa mazingira ni vyema tukazingatia maelekezo ya wataalamu juu ya namna bora ya kukabiliana nayo. Ametoa rai kwa kila mwananchi kuwajibika katika eneo lake kwa kuweka mazingira safi, maeneo yetu tunayafahamu, amesema ikishakuwa kampeni kunakuwa mashindano na nilazima tufanye vizuri ili nasisi tuibuke vinara wa usafi kiwilaya.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa