Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, pamoja na watendaji wa halmashauri wametembelea ujenzi wa Hospital ya karatu. Ziara hiyo ililenga kuona shughuli za mradi wa huo jinsi zinavyoenda.
Ndugu Waziri amesema ujenzi wa hospital hiyo unaendelea vizuri, mpaka sasa majengo yapo katika hatua za umaliziaji wa ujenzi wa msingi. Amesema ujenzi huo wa hospital umeanza mwezi wanne, na unahusisha majengo matatu ambayo ni jengo la Maabara, jengo la wagonjwa wa nje na jengo la utawala. Ujenzi huo unajengwa kwa force account kwa fedha zilizotolewa na hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro. Lengo la ziara hiyo ni kuwapa hamasa mafundi wanaojenga hopitali hiyo. Amesema kufika ijumaaa wanategemea mafundi wawe wameweka jamvi majengo yote matatu.
Ndugu Waziri amesema vifaa vyote vya muhimu vimeshafika eneo la ujenzi. Mpaka sasa tofali 11300 yameshatumika kwa sababu msingi ni mrefu mita moja kwenda chini na tofali zimejengwa kwa kulaza kwenye msingi. Kuna mifuko ya cement zaidi ya 500, mpaka sasa imeshatumika mifuko 1800. Matarajio mwezi wa sita mwishoni majengo yote ya hospitali yatakuwa yameshaezekwa.
Mkurugenzi mtendaji Ndugu Waziri Mourice na watendaji wa Halmashauri katika eneo la ujenzi wa Hospitali ya wilaya.
Karatu District Council
Sanduku la Posta: P.O Box 190
Simu: +255 272970648
Simu ya Mkononi: 0754773947
Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz
Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa