• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UJENZI WA MIUNDO MBINU YA AFYA WASHIKA KASI

Posted on: May 3rd, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Huduma ya maabara, jengo la mama na mtoto na chumba cha kujifungulia ni vipaombele muhimu katika kutoa huduma za afya kwa wananchi. Ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Huduma unaendelea baada ya serikali kutoa fedha shilingi milioni hamsini kwa ajili ya ujenzi. Ujenzi wa zahanati hiyo ukikamilika utawaondolea adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya Rhotia.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea zahanati ya huduma kujionea maendeleo ya ujenzi wa zahanati hiyo. Amesema lazima kamati ya ujenzi ihakikishe huduma ya maji na umeme inakuwepo katika zahanati. Amesema lazima kamati ya ujenzi isimamie fedha za ujenzi vizuri ili ubora wa majengo uendane na thamani ya fedha iliyotolewa.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika zahanati ya kijiji cha huduma

 Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametembelea zahanati ya kijiji cha Kilimatembo ambacho kimetengewa kiasi cha million kumi na Halamashauri ya wilaya ya Karatu fedha ambazo ziko kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha. kiasi hicho cha fedha kitatumika  kumalizia ujenzi wa jengo la zahanati ya kijiji cha Kilimatembo. Ikiwa ni pamoja na kuweka milango na ceiling board, hatua hizo zikienda sambamba na ujenzi wa choo na kichomea taka. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mwenyekiti wa kijiji cha huduma Ndg. Leornad Paulo amesema watazingatia maelekezo yaliyotolewa na serikali, amesema kabla ya ziara hiyo changamoto iliyokuwa inawasumbua ni ubebaji wa mchanga ambayo nayo imeshapatiwa ufumbuzi. Amesema kazi itaenda kwa kasi kwa sababu tayari wataalamu wameshaelekeza eneo la kujenga kichomea taka na  eneo la kujenga maliwato ya nje.

Naye  Mwenyekiti wa kijiji cha Kilimatembo ndg. Nicodemus Said amesema watafanya kila linalowezekana kuhakikisha ujenzi huo unakamilika na wananchi wanaanze kupata huduma za afya katika zahanati ya Kilimatembo. Amesema watatumia msitu wa kijiji ili kupata mbao ambazo zitatumika kuweka milango kwenye zahanati.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika zahanati ya kijiji cha kilimatembo.

matukio katika picha wakati ziara katika zahanati ya kilimatembo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa