• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UKARABATI WA JENGO LA ZAHANATI WAWEKA MASHAKA

Posted on: June 4th, 2019

Kamati ya fedha ya Halmashauri imetembelea zahanati ya kijiji cha Genda, kujione marekebisho ya majengo ya zahanati. Majengo hayo yamejengwa miaka mingi iliyopita, yamepata fedha za Halmashauri kwa awamu mbili ili kufanyiwa ukarabati.

Mhe. Jublate Mnyenye amesema ukarabati wa majengo utekelezaji wake umefanyika vizuri lakini pia kwa upande  mwingine haujafanya kazi vizuri. Majengo ya zahanati hiyo yamepewa million 10 awamu ya kwanza na wamepewa milioni 10 kwa awamu nyingine. Lengo la kufanya ukarabati huo ni kuwekea miundo mbinu mizuri ili iendele kuhudumia vijiji vingine vya jirani. Pamoja na urekebishaji huo bado kuna udhaifu wa fundi anayekarabati jengo hilo kwa kushindwa kuweka mashimo kwenye msingi ili udongo uweze kupumua. Mhe. Mnyenye amesema sakafu inaweka mpasuko kutokana na kukosa mashimo ya kupumua.

Mwenyekiti wa ujenzi zahanati ya kijiji cha Genda Ndugu Paskali amesema kamati ya ujenzi imekuwa haishirikishwi. Hivyo ujenzi huo kuendelea bila ya kamati ya ujenzi; licha ya vifaa kuagizwa na kuletwa eneo la ukarabati wa mradi bila wajumbe kujua hatua za manunuzi, lakini pia namna ujenzi huo unavyofanyika. Wajumbe hao wamemtuhumu Mganga wa kituo hicho Adiael Wilson kwa kufanya shughuli za ukarabati bila kuhusisha kamati ya ujenzi. Kamati hiyo ya fedha imetilia shaka kasi ya ujenzi wa kituo hicho na kumuomba Mganga Mkuu wa wilaya kufuatilia swala hilo kwa undani. kamati hiyo imeelekeza Wajumbe wa kamati ya Ujenzi wa majengo hayo yanayokarabatiwa na Halmashauri kuhakikisha malipo ya mwisho ya mafundi yanalipwa baada ya ukarabati kukamilika na majengo kuwa katika hali nzuri. lakini pia wameagiza kupewa nyaraka, na vielelezo vyote vya namna ukarabati huo unavyoendelea.

Wajumbe wa kamati ya fedha, wakikagua moja ya jengo linaloendelea kukarabatiwa na mafundi.




Matangazo

  • Wasimamizi, Wasaidizi, na Makarani wa Vituo October 06, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

    September 23, 2025
  • WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

    September 23, 2025
  • WENYE SIFA WATAKIWA KUOMBA MIKOPO HALMASHAURI

    September 24, 2025
  • UKUSANYAJI WA MAPATO UNAZIDI KUONGEZEKA KARATU

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa