• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

“UKILA FEDHA MBICHI” UTAZITEMA

Posted on: April 9th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Watendaji wa serikali watakaobainika kutumia fedha za makusanyo ya wananchi kinyume na utaratibu watazirejesha fedha hizo. Serikali imekuwa ikisisitiza kusomwa kwa mapato na matumizi ili kujenga uwazi wa fedha zinazokusanywa kwa wananchi na kuziweka katika akaunti husika ya serikali za kijiji ili kuepusha mianya ya ubadhilifu.

Hayo yamebainika baada ya Mlinzi wa zahanati ya Gongali, kumlalamikia Mkuu wa wilaya Mh. Abbas Kayanda akidai kijiji kushindwa kumlipa Mshahara wake kwa wakati na kusababisha malimbikizo ya Madeni ya  muda mrefu. Hali iliyolazimisha uongozi wa serikali ya kijiji kumpa kwa kumkodisha shamba la kijiji kiasi cha hekari tatu ili kupunguza deni analodai.

Mh. Dastan Panga katika kikao cha kutatua kero za wananchi.

Mh. Kayanda amesema kuna fedha kiasi cha zaidi ya million tano zilizochangwa na wananchi ambazo hazina uwazi wa mapato na matumizi yake. Fedha ambazo kama zingekuwa zimehifadhiwa benki, ingekuwa ni rahisi kwa uongozi wa serikali ya kijiji kumlipa mlinzi wa zahanati pamoja na mlinzi wa ofisi ya kijiji cha Gongali. Mh. Kayanda ameelekeza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kufanya uchunguzi ili kujiridhisha namna fedha hizo zilivyotumika. Kiongozi yeyote wa kijiji atakayebainika kuhusika na ubadhilifu arejeshe fedha hizo na hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yake.

Mh. Kayanda amesema kijiji cha Gongali kimekuwa na mvutano mkubwa kati ya viongozi wa kitongoji na viongozi wa kijiji, jambo ambalo limesababisha shughuli za maendeleo kudorora. Mh. Kayanda ameelekeza viongozi wa kijiji cha Gongali kuhakikisha wanamaliza tofauti zao za kiuongozi  kwa sababu mvutano huo unaumiza  wananchi. Ameongeza kusema tabia za watendaji wachache kufanya ubadhilifu ndio zinazopaka madoa serikali mbele ya wananchi hivyo kufanya wananchi kutokuwa na imani na serikali ya kijiji.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika kikao cha kutatua kero za wananchi kijiji cha Gongali.

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametoa maelekezo mahususi kwa viongozi wa vitongoji kuacha kujihusisha na kuuza ardhi ya kijiji na badala yake uuzaji wa ardhi ufanywe na  serikali ya kijiji ili iweze kupata mapato kama sheria za nchi zinavyotaka. Amesema kumekuwa na ujanja ujanja unaofanywa na viongozi wa vitongoji ya kuuza ardhi kiholela jambo ambalo linanyima kijiji asilimia kumi ya mapato yanayotokana na uuzaji wa ardhi. Amesema sheria za ardhi zinaeleza wazi kwamba ardhi ya kijiji ni mali ya kijiji, hivyo mtendaji wa kijiji na mwenyekiti wa kijiji wanachukua dhamana (madaraka) ya kuidhinisha maafikiano ya uuzaji wa ardhi kulingana na makubaliano yatayokuwa yameafikiwa kati ya mnunuzi na muuzaji kulingana na mipango ya ardhi ya kijiji husika.

Mh. Kayanda amekemea vikali tabia za viongozi wa kijiji kutoza fedha wananchi wenye malalamiko ya ardhi, kufanya hivyo ni kuonea wananchi. Ameongeza kusema uongozi ni dhamana, kama umeomba uongozi ina maana ulikuwa umejitoa kuwatumikia watu na sikuwanyonya au kuwakandamiza watu. Amesema kiongozi lazima afanye kazi kwa mujibu wa kiapo chake wakati anakabidhiwa madaraka ya kuongoza.

Picha katika matukio tofauti wakati wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa