• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UMAKINI WAHITAJIKA UJENZI WA MIUNDO MBINU YA ELIMU

Posted on: January 12th, 2021

 Walimu wakuu na Afisa elimu wametakiwa kujieleza kimaandishi  na kuwasilisha maelezo Ofisi ya Rais Tamisemi juu ya kutofautiana kwa gharama za ujenzi wa mabweni katika shule za sekondari Mang’ola na Domel hasa ikizingatiwa fedha na  ramani ya michoro  kama hiyo  imekamilisha ujenzi katika meneo mengine.

Maelekezo hayo yametolewa Naibu waziri Ofisi ya  Rais Tamisemi Mh. David Silinde alipofanya ziara ya siku moja na kugundua kushindwa kukamilika kwa mabweni shule za sekondari katika tarafa ya Eyasi Karatu. Mh. Silinde ametoa muda wa siku tatu  kwa watumishi hao kujieleza kwanini ujenzi haujakamilika na ametoa maelekezo kwa Injinia wa wilaya kueleza kwanini BOQ imekuwa na gharama kubwa sana tofauti na fedha zilizotolewa na serikali. Samba na maelekezo hayo Mh. Silinde ametaka uchunguzi ufanyike ili kujiridhisha uhalisia wa gharama zilizotumika katika ujenzi uliofanyika.

Mh. Silinde amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli anatoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya elimu  lakini tatizo limekuwa usimamizi dhaifu ngazi ya chini juu ya namna wanavyosimamia ujenzi. Amewataka watendaji kukamilisha ujenzi ili watoto waweze kuingia na ameahidi kurudi kutembelea mwezi wanne.



Mh. David Silinde akikagua ujenzi wa   moja ya bweni katika tarafa  ya Eyasi Karatu


Akizungumza wakati wa ziara hiyo  Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda amemshukuru Naibu waziri ofisi ya rais Tamisemi kwa ziara aliyoifanya wilayani Karatu. Mh. Kayanda ameagiza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa kuanza kuchunguza gharama za ujenzi wa shule hizo ili kubaini kama kuna matumizi mabaya ya fedha katika ujenzi wa miundo ya elimu katika shule hizo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa