• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

USAMBAZAJI WA UMEME VIJIJINI UTAFIKIA MAENEO YOTE

Posted on: August 10th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Wilaya ya karatu ina maeneo 37 ambayo yanapaswa kufikiwa na mradi wa umeme vijijini (REA).  Mpaka sasa kuna maeneo zaidi ya 20 katika wilaya ya Karatu ambayo umeme wa REA haujafika, wakala wa umeme vijijini kupitia kampuni ya NIPO wanatarajia kufikisha umeme kila sehemu ambayo haiujafikiwa  na umeme wa REA ndani ya kipindi cha miezi mitatu.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati akizungumza na wananchi alipotembelea zahanati ya Ngaibara. Amesema anafahamu kuna sehemu ambazo umeme wa Rea haujafika kama kijiji cha Laja, kitongoji cha Baray, Mbuyuni ni miongoni mwa maeneo ambayo umeme wa Rea haujafika . Amesema umeme wa REA utafika maeneo yote wilayani Karatu, Mh. Kayanda ameomba wananchi kutumia mafundi ambao wanatambulika na Tanesco wakati wa  kuweka umeme nyumba zao ili kukwepa mafundi vishoka ambao wanaweza kufanya kazi hizo bila ufanisi. Amewaambia wananchi  wanatakiwa kujaza fomu za kujaza umeme ili wakati wa kusambaza umeme uweze kuwekwa katika makazi yao. wakati huo huo  Mh. Kayanda ametoa maelekezo kwa watendaji wanaosimamia ujenzi wa zahanati ya Ngaibara kuhakikisha miundo mbinu ya maji iwe tayari mpaka kufika alhamisi. Mh.kayanda ametoa siku 10 kuhakikisha ujenzi wa matundu ya choo katika zahanati ya Ngaibara uwe umekamilika.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akikagua ujenzi  wa maabara ya kituo cha afya Endabash.

Mh. Kayanda ametembelea ujenzi wa jengo la maabara katika kituo cha afya Endabash na amejionea ujenzi wa msingi wa maabara. Ujenzi wa maabara utachukua muda wa miezi mitatu mpaka kukamilika kwake na utarajia kuboresha  huduma za upatikanaji wa afya katika kituo cha afya Endabash.

Mh. Kayanda ametembelea ujenzi wa miundo mbinu ya maji Kansay ambayo serikali imeshatoa  Mil 125


za kusambaza maji DP 7 za jamii na kujionea maendeleo ya Mradi.  Mradi huo wa maji utakakamilika mwishoni mwa mwezi wa nane tarehe 30 kwa mujibu wa mkataba. Mh. Kayanda ametemebelea DP ya Shule ya msingi Geer ambayo ina hudumia takribani familia 4414. Ameelekeza  uongozi wa kijiji cha kambi ya Faru kukaa na kuandaa muhtasari utakaosaidia kamati ya maji ya kijiji hicho kuweza kupata nguvu ya kifedha  kununua nishati ya umeme kwa ajili ya kusukuma kwenye matanki ya maji. Ameelekeza kamati ya maji kuhakikisha inarejesha fedha hizo za kijiji kwa wakati na kuhakikisha mradi huo unaweza kujiendesha wenyewe. Mh. Kayanda ameelekeza  wajumbe wa kamati ya maji kutumia muda wa usiku kuvuta maji kwenye tanki ili wananchi waweze kupata huduma ya maji wakati wa mchana.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na wananchi katika Zahanati ya Ngaibara.

Mh. Kayanda amewatahadharisha uongozi wa kijiji kuepuka matumizi mabaya ya fedha au ubadhilifu wowote katika uendeshaji wa mradi wa maji. Amewaasa viongozi kulinda na kutunza miundo mbinu ya maji ili iweze kusaidia wananchi. Amesema kumekuwa na kasumba za matukio ya kuharibu miundo mbinu ya maji kwa kukata mabomba au kutoboa mabomba kwa misumari jambo ambalo linahatarisha  huduma upatikanaji wa maji  na kugaharimu katika kukarabati miundo mbinu ya maji. Amesema atakayebainika kuhujumu miundo mbinu ya maji atakamatwana kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa