• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UTOAJI HUDUMA ZA AFYA WAZIDI KUIMARIKA

Posted on: February 1st, 2021

Na Tegemeo Kastus

Upatikanaji wa dawa katika kituo cha afya Karatu umezidi kuimarika, baada ya vifaaa tiba na madawa ya muhimu kuwepo. Manunuzi ya madawa yaliyofanyika yameleta matumaini kwa wananchi wanaoutumia kituo hicho kama hospitali ya wilaya.

Hayo yamebainika baada ya Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea kituo cha afya Karatu ili kujiridhisha juu ya utoaji wa huduma za afya. Mh. Kayanda amesema amesema  utoaji wa  huduma za afya nzuri ni kipaombele cha kwanza,  hasa ukizingatia kazi kubwa anayofanya Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli katika kuimarisha huduma za afya nchini.

Amesema huduma za afya ikimarishwa vizuri katika kituo cha afya Karatu, itasaidia kuwahudumia wagonjwa wengi wanaotoka Karatu na maeneo ya jirani. Amemuelekeza daktari kiongozi wa kituo hicho kuendelea kufanyia kazi  changamoto zinazojitokeza katika utoaji wa huduma katika kituo hicho.

Katika hatua nyingine Mh. Abbas Kayanda ametembelea zahanati ya Sumawe kujionea maendeleo ya ujenzi wa zahanati hiyo ambayo kwa sasa wananchi kwa kushirikiana na uongozi wa kata ya Ganako wameshajenga choo ambacho kipo katika hatua za mwisho kwa umaliziaji.

Mkuu wa wilaya yaKaratu (kulia) akizungumza na wananchi katika kituo cha afya Karatu

Katika hatua nyingine Bi Laura Bambo amepongeza serikali kwa hatua za ufuatiliaji zinazofanywa na viongozi. Amesema hii inasaidia kuondoa urasimu katika utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. Bi. Bambo amesema utoaji wa huduma za afya unaimarika sana, na kumekuwa na uwazi mkubwa kati ya watoa huduma pamoja na wananchi wanaopata huduma katika vituo vya afya vya serikali.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa