• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA, MAPYA YAIBULIWA

Posted on: March 29th, 2021

Tegemeo Kastus

Udhaifu wa watumishi wa afya wa kutokuwa na rejista ya madawa yanayoingia na kutoka katika vituo vya afya imesababisha upotevu wa dawa za serikali. Hali hiyo imeongeza mwanya wa dawa za serikali kupotea au kuchelewa kuagizwa kwa sababu ya kukosa takwimu sahihi ya kiasi cha dawa zilizoisha na takwimu ya dawa zinazohitajika katika vituo vya huduma ya afya.

Hali hiyo imebainishwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipofanya ziara katika zahanati ya Ayalabe na Tloma katika tarafa ya Karatu. Katika ziara hiyo Mh. Kayanda amefanya ukaguzi wa store za dawa katika zahanati hizo ili kujiridhisha kama dawa zilizopo zinaendana na mahitaji ya kituo. Mh. Kayanda amemuelekeza Mkaguzi wa ndani na Mganga mkuu wa wilaya kufanya ukaguzi wa vituo vyote vya afya ili kujua hali ya upatikanaji wa dawa na ubadhidhilifu wowote utakaoonekana, wahusika warejeshe na hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi yao. Utaratibu wa kukagua dawa katika vituo vya kutolea huduma ya afya utakuwa unafanyika sasa kila baada ya miezi mitatu ili kupata takwimu sahihi za dawa zinazoagizwa MSD na dawa zilizopo katika vituo vya afya.

Mh. Abbas Kayanda katika stoo ya dawa zahanati ya Ayalabe

Mh. Kayanda amekemea tabia za baadhi ya wahudumu wa afya wasio waaadilifu katika kituo cha afya Karatu za kuwaelekeza wagonjwa kununua dawa katika maduka ya watu binafsi. Amesema hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mtumishi yeyote atakayebainika kumuelekeza mgonjwa kununua dawa kwenye maduka binafsi, vitendo hivyo vinaenda kinyume na sera ya serikali ya kuboresha huduma za afya na upatikanaji wa dawa  katika vituo vyote vya afya  ili wananchi waweze kupata mahitaji yote ya kitabibu katika vituo vya afya vya serikali.  Lakini pia kuhamasisha wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa inayowezesha kituo cha afya kuwa na uwezo wa kununua madawa  kwa kujitegemea kulingana na mahitaji.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na wananchi waliokuwa wakisubiria huduma za afya katika zahanati ya Ayalabe

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ameelekeza kuandaliwa kwa utaratibu maalumu wa kuwajulisha  wakinamama wenye watoto wadogo kuja kwa pamoja kupata chanjo ya polio kwa watoto wao badala ya utaratibu wa kuwaacha kuhudhuria kliniki kwa uchache kwa ajili ya kupata chanjo ya polio. Amesema chupa moja chanjo inahitaji kutumika kwa watu 17 hivyo kufungua chupa kwa watu wachache ni kuharibu chanjo hizo.

Wakati huo huo Mh. Kayanda amemuelekeza mganga Mkuu wa wilaya kushughulikia swala la malipo ya walinzi katika zahanati ya Ayalabe na Tloma waliokuwa wanadai malikimbizo ya mishahara. Ikiwa nipamoja na kuandaa utaratibu wa kuwaweka kwenye bajeti ili kuondoa changamoto ya malimbikizo ya madeni inayojitokeza mara kwa mara katika zahanati hizo.

Mh. Kayanda ameelekeza utaratibu ufanyike ili nyumba za wafanyakazi wa afya katika zahanati ya Tloma ziweze kupata huduma ya umeme. Katika ziara hiyo Mh. Kayanda ametembelea zahanati ya Gyekrum Arusha kujionea hali ya utoaji wa huduma katika zahanati hiyo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa