• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

UZINDUZI WA UOGESHAJI WA MIFUGO WAFANYIKA ENDABASH

Posted on: December 17th, 2018

Na Tegemeo Kastus

Uzinduzi wa uogeshaji wa mifugo Umefanyika kimkoa jana katika kijiji cha Endabash Tarafa ya Endabash. Zoezi lilihusisha wataalamu wa mifugo wa Mkoa wa Arusha sambamba na wataalamu wa mifugo wa Wilaya ya karatu. Mgeni rasmi katika ufunguzi wa zoezi hilo ni Mkuu wa wilaya ya Karatu Mheshimiwa Theresia Mahongo.

Katika hotuba yake ya uzinduzi Mheshimiwa Theresia Mahongo amesema wilaya ina majosho 26  na majosho 3 ndio yanafanya kazi. Mkoa wa arusha una ng’ombe 1,859,404 wilaya ya karatu ina ng’ombe 166,157 ina mbuzi 258,729 ina kondoo 85,997 takwimu ni kutokana na zoezi la upigaji chapa mifugo. Mheshimiwa Theresia amepongeza wafugaji na wanakijiji wa Endabash kwa kukarabati josho la mnadani, amesema katika soko la mifugo ambalo lipo wilaya ya Longido Namanga mifugo mingi inayouzwa katika soko hilo inatoka wilaya ya Karatu. Ameomba wananchi wasipite njia za mkato kwenda kuuza mifugo ili serikali iweze kuongeza mapato.

Mheshimiwa Theresia  Mahongo amesema katika kutekeleza ilani ya chama cha mapinduzi, serikali imetoa dawa kwa ajili ya kuogesha mifugo kwa majosho yote yanayofanya kazi. Mheshimiwa Theresia amesema Waziri Wa Mifugo Mheshimiwa Luhaga Mpina 7/12/2018 katika mkutano wa Madakatari wa  mifugo uliofanyika nchi nzima  Arusha aliagiza majosho yote yaliyo kwenye Halmashauri yanakarabatiwe. Mheshimiwa Theresia amesema serikali imetoa dawa ya kuanzia kuogesha mifugo hivyo kamati za majosho zikae zipange bei za uogeshaji mifugo ili kuweza kununua dawa, wakati wa kupanga bei ni vizuri kushirikisha wafugaji. Amesema ni marufuku  kwa wafugaji kufika kwenye josho na kuosha kinyemela na kinyume na ratiba zitakavyopangwa.

Mheshimiwa Theresia amesema mifugo inatakiwa kuogesha mara mbili wakati wa kiangazi na wakati wa masika mara tatu. Amehimiza Kamati ya majosho kuwa waadilifu hasa katika matumizi ya fedha za uogeshaji. Mheshimiwa Theresia amesema kamati za majosho zisimamiwe na serikali ya kijiji kufungua account maalumu ya benki, waweka sahihi wawili watoke serikali ya kijiji na wawili kamati ya majosho. Mh. Theresia ameagiza kamati ya majosho kusoma taarifa za mapato na matumizi kwenye serikali ya kijiji. Fedha za majosho zitumike kuendeleza majosho na ratiba za uogeshaji zisiwe na upendeleo, ameelekeza watendaji kupanga utaratibu mzuri wa uogeshaji wa mifugo  kwa vijiji visivyo na majosho. Mhe Theresia ameonya watu watakao hujumu miundo mbinu ya majosho hatua kali zitachukuliwa dhidi yao, ameelekeza kamati za vijiiji kusimamia ulinzi wa majosho.

Mheshimiwa Theresia amesema dawa za ruzuku zitakapoisha wafugaji waendelee kuchangia dawa. Amewaagiza maafisa mifugo pamoja kamati ya Majosho waandike taarifa za dawa wakati wa kubadilisha na taarifa ziende kwa mkurugenzi. Amewaonya wafugaji wanaokwepa kulipa mapato wakati wanapouza mifugo mnadani amesema Karatu itajengwa na wanakaratu wenyewe, ameomba Maafisa mifugo kutekeleza majukumu yao vizuri.



Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa