• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI, TUWE NA UELEWA MMOJA JUU YA MKAKATI WA KUBORESHA UTALII

Posted on: July 4th, 2019

Mpango mkakati wa kuboresha fursa za maeneo ya utalii ya ziwa Eyasi, na kuchangia maendeleo endelevu umewasilishwa katika Ukumbi wa Halmashauri. Mpango mkakati huo umesomwa ili kupata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wataalamu wa Halmashauri na viongozi wa wilaya.

Mpango mkakati huo umeanzishwa kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Karatu unaendeshwa na UCRT na VSF ya Ubeligiji ili kuboresha usimamizi wa maeneo ya utalii kwa kufanya  uchambuzi halisi kuangalia uwezo na udhaifu ili kupata mwelekeo wa kimkakati wa utalii kwa miaka mitano ijayo.

 Mgeni rasmi katika uwasilishaji huo, Mhe. Theresia Mahongo amesema mpango wa utalii wa miaka mitano ni mzuri. Amesema mpango umegusa matatizo yote katika mpango mkakati wa kuboresha utalii wa Eyasi. Amesema ni vyema kuhamasisha watu juu ya mpango mkakati wa utalii ili tuweze kwenda wote kwa pamoja. Mhe. Theresia amesema tunapaswa tuwe na tafsiri nzuri ya uboreshaji utalii wa kitamaduni tunapowaeleza wananchi. Amesema ni vizuri viongozi tuwe na uelewa mmoja juu ya Mpango mkakati wa kuboresha utalii ili tuweze kujenga hoja za kuwafahamisha wananchi.

 Naye Mbunge wa Karatu, Mhe. Willbroad Qambalo amesema sisi kama wadau, mpango mkakati huu si Msaafu wala Bibilia. Amesema tunaweza kujiwekea namna ya kufanya mapitio juu ya mpango mkakati huo kila mwaka kama kuna uhitaji wa kufanya marekebisho. Amesema baada ya kupitisha mpango mkakati huo sasa kwenye kuweka kanuni ndio kila mtu anayehusika na utalii wa utamaduni Tarafa ya Eyasi aje na hoja anahitaji kiasi gani kwenye tozo.

Mhe. Willbroad Qambalo wakati akichangia mjadala.

Mhe. Qambalo ameongeza kusema hali ikiendelea kama jinsi ilivyo sasa utalii wa kitamaduni utakufa Tarafa ya Eyasi. Amesema lazima tuende sawa, kuna kitongoji cha Murus kinapokea watalii sana na kuna kambi tatu za wahadzabe lakini hawajajumuishwa katika mpango huo.  Kitongoji cha Murus hawapo Tarafa ya Eyasi lakini kina maeneo matatu mazuri yanayojihusisha vizuri na utalii wa kiutamaduni. Amesema mpango mzuri wa ardhi lazima utekelezwe, maeneo yale ya utalii yahifadhiwe ili wahadzabe wanaotegemea uwindaji waendelee na shughuli zao badala ya kusubiri utalii.

Katika uwasilishaji wa maoni, Mwenyekiti wa Halmahauri Mhe. Jublate Mnyenye amesema lazima tuweke utaratibu wa kupanda miti na kuacha shughuli za kuchoma mkaa na kukata miti hovyo. Amesema kwenye tozo, swala la kubadilisha fedha za kigeni, wenyeji watoe fedha za kitanzania na kwa wageni watumie malipo ya fedha za kigeni. Amesema waongoza utalii ukiwapa mwanya wa kutumia malipo ya fedha za kitanzania tutaweka mwanya kwa waongoza utalii kufanya biashara ya kubadilisha fedha za kigeni. Amesema upo umuhimu wa kuwashirikisha TATO katika mpango huu wa kuboresha utalii wa kitamaduni wilayani Karatu. Amesema Halmashauri ni msimamizi wa shughuli za utalii na shughuli za maendeleo, hatupaswi kuwatenga katika mpango mkakati.

Awali Ndugu Dismas Meitaya   Program and Codinator   UCRT -Ujamaa Community Resouce Team, wakati akiwasilisha amesema andiko lao limelenga kukuza utalii wa kitamduni unao adimika. Amesema mkakati umejikita katika Uhifadhi wa mazingira unaoboreshwa ustawi wa kiuchumi na na ubora wa maisha ya jamii.

Amesema wameangalia maadili ya tamaduni za kitalii na kuangalia vivutio vyote vya utalii Tarafa ya Eyasi, pamoja na pendekezo la malipo ya utalii. Amesema katika utafiti wa andiko wamebaini kumekuwa hakuna uhalisia katika uonyeshaji wa utamaduni. Amesema katika utafiti wameona kumekuwa na changamoto ya kukosa uwazi na uwajibikaji katika ukusanyaji wa mapato na kumekuwa na madhaifu ya miundo mbinu inayohusiana na shughuli za kitalii katika eneo la utamaduni wa kitalii. Amesema kumekuwa pia na tabia zisizo za kimaadili kwa waongoza utalii wa kijamii. Ndugu Dismass amesema rasimu mpango ikikubalika, utaandikwa vizuri ili uweze kusainiwa kama mpango makakati wa kuboresha utalii wa utamaduni Tarafa ya Eyasi.


Watendaji na Viongozi wakifuatilia uwasilishaji wa Mpango mkakati wa kuboresha utalii wa kitamaduni Tarafa ya EYasi

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa