• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

VIONGOZI WA KINIHHE NA QARU WAMALIZA TOFAUTI ZAO

Posted on: August 29th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Serikali imewataka wananchi wa vijiji vya Qaru na Kinihhe  kudumisha umoja na mshikamano ili kuchochea ujenzi wa miradi ya maendeleo. Viongozi mmepewa dhamana ya kuongoza lazima muwe mfano katika kuongoza wananchi kwa kutekeleza maamuzi halali ya vikao vya Halamashauri kuu  ya kijiji. Ni jukumu la viongozi kutafuta ufumbuzi wa pamoja kwa njia ya majadiliano  na kuridhiana pindi inapotokea utofauti wa kimtazamo katika kuongoza.

Mh. Kayanda akiwa katika kikao cha ndani  na wajumbe wa Halmashauri  vijiji vya Qaru na Kinihhe

Hayo yamejiri katika kikao cha ndani cha Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda na wajumbe wa Halmashauri ya viijiji vya Qaru na Kinihhe. Katika kikao hicho Mh. Kayanda amesisitiza umuhimu wa viongozi kukaa pamoja na wataalamu wa ardhi ili kukusanya maoni juu ya mvutano wa mpaka kati ya kijiji mama Qaru na kijiji cha kinihhe ufanyike, kupitia vikao vya Halmashauri kuu ya vijiji vya Qaru na Kinihhe. Ili baada ya hapo mapendekezo yapelekwe katika vikao vya maendeleo ya kata kwa ajili ya kupata ufumbuzi wa kudumu.

Kuhusu swala la kugawana mali zilizozalishwa kwa pamoja kabla ya kijiji cha Kinihhe hakijajitenga kutoka kijiji cha Qaru mwaka 2009. Mh. Kayanda ameelekeza viongozi wa serikali ya kijiji cha Kinihhe  kuandika barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashuri ya Karatu na nakala kwenda katibu tawala wa wilaya ya Karatu wakiomba kuundwa kwa kamati ya mgao wa mali ili kuwezesha taratibu za mchakato wa kugawana mali kuanza.

Wajumbe wa serikali za vijiji vya Qaru na Kinihhe kwenye katika kikao cha ndani

Katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kinnhe Mh. Kayanda amehimiza wananchi kuendelea kudumisha mahusiano mazuri na kijiji mama cha Qaru. Amesema mivutano inachelewesha kasi ya ujenzi wa miradi ya maendeleo. Ameelekeza Meneja wa tanesco wilaya ya Karatu, kufanya tathimini kwenye kijiji cha kinihhe kwa ajili ya kukiweka kijiji hicho kwenye mpango wa usambazaji wa umeme vijijini (REA) mwaka ujao wa fedha.

Wakati huo huo Mh. Kayanda amemuelekeza Mganga Mkuu wa wilaya ya Karatu kufanyia tathimini na kuliweka jengo la zahanati ya kijiji cha kinihhe katika mpango wa bajeti ya Halmashauri ili jengo la zahanati hiyo liweze kukamilika na lianze kutoa huduma. Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ameelekeza wataalamu wa ardhi wa wilaya kwenda kupima eneo la chanzo cha maji kinachohudumia vijiji vya Qaru na Kinihhe, ili kujua ukubwa wake halisi baada ya kuwepo taarifa kuwa eneo hilo limevamiwa  na shughuli za kibinadamu zinafanywa ndani ya chanzo cha maji. Amesema kufanya shughuli za kibinadamu kwenye eneo la chanzo cha maji kisheria ni makosa. Amemuelekeza Afisa tarafa wa Endabash kwenda kulitembelea eneo hilo la chanzo cha maji na kulitolea taarifa ofisi ya mkuu wa wilaya.

Mwenyekiti Ndg. Vicent Gabriel   akifungua Mkutano wa hadhara

Akizungumzia kuhusu swala la wanafunzi kupata chakula shuleni, Mh. Kayanda amesema mpango huo ni mzuri na unalenga kuboresha maendeleo ya kitaaluma. Amesema kama vikao vya Halmashauri ya vijiji vilikaa na kukubaliana wazazi wachangie chakula cha wanafunzi shuleni basi serikali za vijiji hazina budi kusimamia maamuzi halali ya vikao vya Halmashuri ya kijiji. Amesema serikali ya kijiji cha Qaru ikae na iweke msukumo kwa wanafunzi wanaosoma katika shule ya msingi Qarulambo na sekondari ya Qaru wawe wanapata chakula cha mchana shuleni, halikadhalika serikali ya kijiji cha Kinihhe isimamie wazazi wa kijiji hicho ili kuhakikisha wanafunzi wanaosoma shule ya msingi QaruLamabo na sekondari Qaru wawe wanapata chakula cha mchana shuleni.

Awali katika Mkutano wa hadhara Mwenyekiti wa kijiji cha Kinihhe Ndg. Vicent Gabriel alisema kulikuwa na mvutano mkubwa na kijiji mama cha Qaru. Hivyo kusababisha wananchi kususia kujitolea nguvu kazi na michango kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari Qaru. Amesema sababu kubwa ni mabishano ya mpaka, amesema wananchi wa Kinihhe walikuwa  wananung’unikia kutopewa mgao wa mali kutoka kijiji mama cha Qaru.

Wananchi wa kijiji cha Kinihhe wakiwa katika mkutano wa hadhara

Ndg. Gabriele amesema hata kijiji cha Qaru kilikuwa na manung’uniko juu ya kutofautiana kuhusu mipaka halisi ya inayotenganisha vijiji vya Qaru na Kinihhe. amesema maelekezo ya Mkuu wa wilaya yameleta usawa na kuondoa malalamiko ya muda mrefu yaliyokuwa yanazorotesha maendeleo katika kijiji cha Kinihhe na kijiji cha Qaru. Amesema sasa wamefungua ukurasa mpya na wameweka tofauti zao pembeni. Ndg. Gabriel amehimiza swala la wananchi kujitoa nguvu kazi katika kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo. Amesema wajumbe wa Halmashuri ya kijiji cha Kinihhe wanatakiwa kukamilisha  mchango wa 36000 itakapofika 20/9/2021 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Qaru  kama walivyokubaliana katika vikao vya Halmashauri ya kijiji huku wananchi wa kijiji hicho wakitakiwa kukamilisha mchango wa  kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa ifikapo tarehe 20/10/2021. Amesema kijiji cha Qaru kimefika katika hatua nzuri katika kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari Qaru. Ujenzi wa vyumba vya madarasa ni jitihada za serikali za vijiji vyote viwili katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madarasa katika shule ya sekondari Qaru inayotarajia kupokea mwakani, makisio ya wanafunzi 190 wa kidato cha kwanza kutoka kwenye vijiji vya Qaru na Kinihhe.

Mh. Kayanda akikagua jengo la zahanati ya Kinihhe 

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa