• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MSISITIZO WAWEKWA UANDIKISHAJI MFUKO WA BIMA YA AFYA YA JAMII ULIOBORESHWA

Posted on: September 9th, 2021
  • NA TEGEMEO KASTUS

Waratibu wa afya waelekezwa kuandaa mpango kazi mzuri ambao utasaidia kuongeza idadi ya wananchi wanaojiunga mfuko wa bima ya afya ya jamii ulioboreshwa. Zoezi la kuratibu shughuli za uandikishaji lazima uhusishe viongozi wa siasa, viongozi wa dini na asasi za kiraia ili kujenga uelewa wapamoja kwa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na bima ya afya ya jamii ulioboreshwa.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda katika kikao cha kamati ya afya ya msingi (DPHC) kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri. Mh. Kayanda amesema uandikishaji wa wananchi katika mfuko wa bima ya afya ya jamii  ulioboreshwa bado uko chini, na uelewa wa watu juu umuhimu kujiunga na mfuko wa bima ya afya bado ni mdogo. Amesema wilaya ya Karatu ina kaya 45, 000 lakini kaya zilizojiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa ni kaya 2600, amesema lengo la serikali ni kuhakikisha  kila mwananchi anakuwa na uhakika wa matibabu. Mh. Kayanda amewapongeza wadau wa maendeleo shirika la food for his children kwa kusaidia kuandikisha katika mfuko wa bima ya afya ya jamii ulioboreshwa kaya 324 katika Halmashauri ya wilaya ya Karatu.

Mh. Kayanda akizungumza katika kikao cha kamati ya afya ya msingi

Mh. Kayanda amesema watu wanavyoozidi kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya jamii ulioboreshwa unasaidia kujengea uwezo vituo vya afya katika kununua dawa. Ameongeza kusema ni vyema wataalamu wa afya wakainisha kwenye mbao za matangazo, aina za dawa zinazopatikana katika vituo vya afya ili kuondoa malalamiko juu ya ukosekanaji wa dawa katika vituo vya afya. 

Mh. Kayanda ameelekeza wataalamu wa afya kufuata miongozo ya afya wakati dawa zinapoletwa kutoka bohari ya dawa (MSD) na kukabidhiwa kwenye vituo vya afya kwa kuhusisha kamati ya afya za vituo. Amesema wajumbe wa kamati hizo ndio wanasaidia kuelewesha wananchi juu hali ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya. ameongeza kusema katika swala la utoaji wa dawa lazima taratibu za kujaza daftari la rejesta ya dawa ufuatwe, ili kuwezesha vituo vya kuwa na taarifa nzuri za matumizi ya dawa kwenye vituo lakini kusaidia kudhibiti vitendo vya upotevu wa dawa kwenye vituo.

Matukio katika picha wakati wa kikao

Akizungumzia kuhusu usafi wa mazingira ameelekeza watendaji kuja na mpango madhubuti wa kuhamasisha wananchi kujenga vyoo.  Amesema ili kuongeza ufuatiliaji katika ujenzi wa vyoo bora ni lazima viongozi na watendaji wa ngazi zote kwenye maeneo yao ya utawala kuhusishwa vizuri katika kuweka msisitizo na kufanya ufuatiliaji.  

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda amezungumzia juu ya usimamizi wa usafi katika mji wa Karatu ambao unafanyika kila jumamosi ya mwisho wa mwezi. Ameelekeza juhudi zaidi zifanywe na wataalmu wa idara ya usafirishaji na mazingira ili kuweka mji wa Karatu katika hali ya usafi. Ameongeza kusema mji wa Karatu ni mji unaojihusiha na shughuli za utalii amesema lazima kuwe na mkakati  maalumu wa kusimamia usafi na kuhakikisha mji unakaa katika hali ya usafi.

matukio katika picha wakati wa kikao cha kamati ya afya ya msingi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa