• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WADAU, TUPAZE SAUTI JUU YA ELIMU YA AFYA

Posted on: April 4th, 2019

Wadau wa afya wilaya ya Karatu wanafanya mkutano wa siku mbili, kuanzia leo kujadili mambo mbalimbali yanayohusiana na sekta ya afya. Mkutano huo umefunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu.

Mhe. Theresia amewashukuru wadau wa afya BORESHA AFYA  na wadau wengine kwa kujitoa kusaidia maswala ya afya. Amehimiza wadau wa afya kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU). Kwenye mapambano dhidi ya VVU tumejisahu ndio maana hatufanyi vizuri, amehimiza wadau wa afya kuendelea kupaza sauti ili kukabiliana na maambukizi vvu.

Mhe. Theresia amesema Karatu  tunapata wageni wengi kutoka sehemu mbalimbali, ni vyema kuendelea kuwapa watu elimu juu ya maambukizi ya virusi vya ukimwi. Amesema shule ya sekondari ya Welwel ni shule ya kutwa na baada ya mida ya masomo wanafunzi wanarudi nyumbani. Zipo taarifa zinazoonyesha wanafunzi wa shule hiyo kujihusisha na tabia hatarishi. Amemuelekeza Mwenyekiti wa Halmashauri kuliangalia swala la shule ya sekondari welwel, tunawahitaji watoto hawa  kwa ustawi wa taifa. Kuwapoteza watoto hawa ni hasara kwa taifa.

Mhe. Theresia amehimiza pia swala la elimu ya lishe, ameomba wadau wa afya kutoa elimu ya lishe mpaka shuleni. Kuna uelewa mdogo juu ya elimu lishe, tutoe elimu lishe kwa wakinama wanapoenda clinic ili wapate uelewa wa pamoja.

Mhe. Theresia amesema pia kuna uhitaji mkubwa wa elimu kwa wananchi juu ICHF iliyoboreshwa. Bima ni msaada mkubwa kwa wananchi, kwa sababu inawapa uhakika wa matibabu wananchi.

Awali katika taarifa yake Mganga Mkuu wa wilaya, Dkt Mustafa Waziri amesema wanachangamoto ya wakinamama kujifungulia nyumbani.  Mwaka 2018 kama wilaya tulikuwa na kiwango cha 61 % ya kiwango cha wakinamama waliojifungulia katika vituo vya kutolea huduma na lengo la serikali ni kufikia 80%.

Dkt Mustafa amesema wanachangamoto pia katika swala la uzazi wa mpango, mwaka 2018 tulikuwa na kiwango  cha 44 % na lengo la serikali ni  kufikia 60%. Dkt.Mustafa amesema kuna kaya 45065 na kaya zilizojiunga mwaka 2018 ICHF iliyoboreshwa  ni kaya 14255 ambayo ni sawa 31%. Changamoto kubwa ilikuwa ni kukosa vitendea kazi. Dkt Mustafa amesema mpaka sasa wamepokea simu 32 kwa vituo vyote 32 na watu watakohusika na undikishaji wameshateuliwa hivyo wanatarajia sasa kuongeza idadi ya watu watakao jiunga.

Dkt. Mustafa amesema upatikanaji wa dawa mwaka ( 2018 )  ulifikia 97.9 % , pia wameweza kukusanya damu salama chupa zaidi 1250. Amesema vituo vyote vya serikali na binafsi vinavyofanya operation vinatumia damu iliyokusanywa.

Wajumbe waliohudhuria kikao cha wadau wa afya.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao cha wadau wa afya.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa