• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WADAU WA ELIMU WAKABIDHI BWENI SEC-KILIMAMOJA

Posted on: September 26th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Wafadhili wa Africa foundation wamekabidhi kwa serikali ujenzi wa bweni la wavulana na jengo la choo cha wasichana vienye thamani ya pamoja zaidi  ya million 113 kwa shule ya sekondari kilimamoja. Bweni la wavulana lina uwezo wa kubeba wanafunzi 64 litakuwa msaada kwa wanafunzi wanaotoka mbali na eneo la shule.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda amewapongeza wafadhili hao kwa msaada waliotoa kwa shule ya sekondari kilimamoja. Amesema wadau wa elimu kazi wanayofanya ni kuunga mkono kazi kubwa iliyofanywa na Mh. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuimarisha miundo mbinu katika shule ya msingi na sekondari. Amesema serikali imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji na mambo haya wanayoyafanya wawekezaji hawa ni kurudisha shukrani kwa jamii.

Mh. Abbas Kayanda akikagua bweni la wavulana kwa ndani.

Muonekano wa bweni la wavulana kwa nje.

Mh. Kayanda amesema muwekezaji Africa foundation anaamini kabisa njia pekee ya kuikomboa jamii ni kuwekeza katika elimu. Amesema elimu inatoa maarifa ambayo yakiingia kichwani  hayawezi kupotea. Amewaasa wanafunzi kusoma kwa bidii ili elimu yao ije kusaidia jamii, amesema ili mwanafunzi aweze kufikia malengo yake lazima awe na nidhamu. Lazima miundo mbinu iliyojengwa ichochee kiwango cha ufaulu wa wanafunzi. Amesema mabadiliko ya kitaaluma ndio yatakayoonyesha umuhimu wa miundo iliyojengwa.

Mh. Kayanda ametoa wito kwa walimu kusimamia na kuhakikisha miundo mbinu inadumu kwa muda mrefu,  lakini kuchukua hatua stahiki kwa mtu yeyote atakayeharibu miundo mbinu. Amewaasa wanafunzi kuwa na nidhamu ya matumizi ya miundo mbinu iliyojengwa na kila mwanafunzi kuwa mlinzi wa mwenzake.

Mh. Abbas Kayanda (kulia) akizindua jengo la choo cha wasichana sekondari ya Kilimamoja.

Mh. Abbas Kayanda akikagua jengo la choo cha wasichana sekondari ya Kilimamoja.

Awali Afisa elimu sekondari Bi, Kalista Maina amesema bweni lilojengwa litasaidia wanafunzi kupunguza utoro wa mara kwa mara na vishawishi mbalimbali. Amesema bweni hilo litawaongezea umakini wa kusoma kwa bidii ili waweze kutimiza malengo yao. Amesema bweni litasaidia wanafunzi kupata muda mwingi wa kujisomea wakati wa usiku lakini  kuwaondolea wanafunzi uchovu wa kutembea  umbali mrefu kutoka nyumbani.Bi.Maina ameomba wazazi kuwajibika kwa watoto wao kwa kuhakikisha wanapatia wanafunzi mahitaji yote muhimu kwa wakati.

Naye Mkurugezni wa Africa Foundation Dkt. Ernest Mgono amesema shule ya sekondari kilimamoja ipo karibu na maeneo ya hifadhi na maeneo hayo ya hifadhi,  amesema katika maeneo hayo ya uhifadhi ndipo walipoweka vitega uchumi vyao. Hivyo  kwa kuwa katika maeneo waliyowekeza kuna jamii inawazunguka lazima jamii ipate faida kidogo ili waendelee kujali na kutunza hifadhi.

Dkt. Mgono amesema walishaanza kujenga bwalo la chakula lakini wameshajenga bwala la wanafunzi wa kike kabla ya kukabidhi bwalo la wanafunzi wa kiume. Amewaomba wanafunzi kutunza  majengo yote yaliyojengwa  ili majengo hayo yaweze kudumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa