• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAFANYAKAZI ONGEZENI UFANISI

Posted on: May 1st, 2019

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi yamefanyika kwa maandamano ya amani na kupokelewa na Mhe.  Theresia Mahongo Mkuu wa wilaya ya Karatu katika uwanja wa mazingira bora. Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi ni “ Tanzania ya uchumi wa kati inawezekana, wakati wa mishahara  bora kwa wafanyakazi ni sasa.

Mhe. Theresia amewapa zawadi watumishi waliofanya kazi vizuri katika maeneo yao ya kazi, na  amewapongeza waajiri kwa kutoa motisha kwa wafanyakazi. Mhe  Theresia amewaelekeza waajiri kulipa kwa wakati mifuko ya hifadhi ya jamii kwa watumishi. Amewataka waajiri kulipa madeni ya watumishi, amesema malalamiko ya watumishi kutolipiwa na wajiri wao katika mifuko ya hifadhi ya jamii yanaongezeka. Mhe Theresia ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi mtendaji wa wilaya kutoa barua za miongozo ya kazi (job description) kwa watumishi wote ili watu wajue wajibu wao katika maeneo yao ya kazi. 

Mhe. Theresia amesema serikali imeendelea kuweka mazingira mazuri kwenye maeneo ya kazi kwa kuhakikisha mishara ya wafanyakazi inalipwa mapema, amesema kwa mkoa wa Arusha serikali inalipa billion 179 mshahara wa wafanyakazi. Serikali imeajiri watumishi na Karatu imepata walimu wapya  27 na madaktari 32 kwa mwaka huu wa fedha. Serikali kwa mwaka wa fedha 2017-2018 imepandisha madaraja watumishi 1017 kati yao walimu ni 750. Mwaka wa fedha 2018-2019 serikali itapandisha madaraja watumishi 2132   kati yao walimu ni 1542. Serikali imelipa madeni ya walimu mwezi February na March mwaka huu shilingi million 52 posho za uhamisho pamoja na likizo.

Mhe. Theresia amewataka watumishi kutoa huduma bora kwa wananchi, kwa taarifa zinazotolewa na Takukuru bado Halmashauri, Mahakama zinaongoza kwa rushwa. Amewataka wafanyakazi kupambana ili kutoa haki kwa wale wanaowahudumia, hakuna haki bila wajibu. Mhe. Theresia amesema mwaka huu ni mwaka wa uchaguzi wa serikali za mitaa, amewataka watumishi kusimamia zoezi hilo vyema kwa kuwapa wananchi elimu juu ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Amewashukuru watumishi kwa kuendelea kulinda amani ameomba watumishi kuendelea kuwa na subira, juu ya ongezeko la kima cha mishahara amesema subira yavuta kheri.

Katika risala ya wafanyakazi iliyosomwa na ndugu Florence Mollel, wameomba serikali, kupunguza utofauti mkubwa wa maslahi kati ya mtumishi wa ngazi ya chini na mtumishi wa ngazi ya juu. Amesema maslahi ya kazi za kisiasa yamekuwa mazuri zaidi ya watendaji wa kawaida wa serikali. Hii imefanya wataalamu wengi kufikiria kwenda kwenye shughuli za kisiasa na hivyo kuathiri  shughuli za kitaalamu.

Ndugu Florence amesema uingiliano wa siasa kwenye utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo ambao unakwamisha sera za serikali, dira maendeleo 2020-2025, Maendeleo endelevu ya  2030 na  Mipango ya mandeleo ya miaka 5  na ilani ya chama cha mapinduzi ya 2015-2020 kuathiriwa wakati wa utendaji.

wafanyakazi wakifuatilia kwa makini maadhimisho ya may mosi Uwanja wa Mazingira Bora.

Mmoja wa wafanyakazi aliyepewa zawadi ya may mosi Uwanja wa mazingira Bora.


Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa