• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAKINAMAMA WAJASIRIAMALI WANUNUA VIWANJA VITATU

Posted on: February 9th, 2019

 Kinamama wajasiriamali wa kikundi cha Juhudi na Kujitegemea Wilayani Karatu, wamekuwa mfano kwa vikundi vingine kwa kukuza na kuimarisha mradi wa kuuza maziwa ya ng’ombe. Hayo yamesemwa na Mratibu wa vikundi vya kinamama Bi, Adela Shauri alipokitembelea kikundi hicho mwishoni mwa wiki.

Halmashauri ya wilaya ya Karatu iliwapatia mkopo kinamama hao pamoja na elimu ya ujasiriamali kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii. Mkopo ambao umewasaidia kinamama hao kujikwamua kiuchumi kwa kuongeza wigo wa kipato chao.

Kikundi kilianza katika kijiji cha Gongali lakini kutokana na hitaji la kuwafikia wateja wa maziwa kwa urahisi walihamisha mradi kwenda Karatu mjini. Bi, Martha Panga, ambaye ni Mhasibu wa kikundi hicho anasema kikundi kina jumla ya wanachama kumi walianza mwaka 1995, wakijishughulisha na kufyatua matofali.

Bi, Martha anasema awali walikuwa wanafanya mikutano yao chini ya mti katika kijiji cha Gongali na kukopeshana wenyewe kwa wenyewe. Walianza na shughuli ya kufyatua matofali ambayo ilikuwa ngumu ikawashinda; wakaamua kutengeneza pombe ya kienyeji, ambayo pia iliwashinda kutokana na pombe kuchachuka. Bi Martha anasema waliamua kujishughulisha na  kilimo, walilima wakapata mahindi gunia sita na kipindi hicho gunia la mahindi lilikuwa linauzwa shilingi elfu nne. Wakaanza kukopeshana wenyewe kwa muda wa miezi mitatu mpaka sita ili kukuza mtaji na mtu wa kwanza waliyemkopesha walipata elfu arobaini, mtu wa pili wakapata elfu thelathini na mtu wa tatu wakapata elfu kumi kitu ambacho kiliwasaidia  kurudisha riba.

Bi Martha anasema Halmashauri ya Wilaya ya Karatu iliwapeleka semina Tengeru walienda kujifunza kuhusu usindikaji na baadae Halmashauri iliwaasaidia kupata elimu ya ujasiriamali na wakafanikiwa kupata mkopo wa million moja na nusu. Bi Martha anasema mkopo huo haukuwa fedha taslimu bali walinunuliwa vifaa kama mashine ambayo ni Cream separator, Makeni, na Masufuria. Bi Martha anasema waliweza kurudisha mkopo kutokana na shughuli zao za kugandisha maziwa walizokuwa wameanza.Wanakikundi walianza kwa kugandisha lita ishirini, baadae lita arobaini, baadae lita hamsini na mpaka sasa wanagandisha lita mia na hamsini.

Bi Beatha Yotham ambaye ni mmoja wa wanachama anasema malengo ya mradi wao ni kuwawezesha kujikwamua kutoka kwenye maisha duni. Bi Beatha anasema wamefanikiwa kununua viawanja vitatu, ambacho kimoja wamenunua million tano, kiwanja kingine Million nane na kiwanja cha tatu walinunua kwa shilingi elfu hamisini. Wameweza kujenga nyumba katika kiwanja kimoja na wamepangisha wapangaji wawili. Lakini pia wamefungua mradi wa pili wa maziwa Stendi ya Karatu unao wagharimu kama million tatu kwa mwaka kama kodi ya pango. Lengo lao ni kuwasogezea wateja wao huduma karibu, lakini pia kutokana na shughuli zao  Halmashauri imewapa mkopo tena wa million kumi  kwa ajili ya kuboresha shughuli zao.

 Bi Beatha anasema changamoto kubwa kwao kwa sasa ni wakati wa kipindi cha baridi ambacho kiasi kikubwa cha maziwa kinabaki bila kununuliwa. Wenyewe kama wanakikundi wanaona wakipata mtungi  mkubwa wa kuhifadhia  maziwa wakati baridi utawasadia. Bi Beatha  anasema wao hawana vifungashio imara kwa ajili kufungia Siagi, wanaona wakipata vifungashio imara itaongeza thamani zaidi ya bidhaa zao. Bi Beatha anasema  wanachangamoto ya usafiri kwa ajili ya kukusanya maziwa wakati wa kiangazi, kwa sababu ya uhaba wa upatikanaji wa  maziwa hivyo wakipata usafiri wa uhakika utawasaidia kukusanya maziwa kwa urahisi.

Bi Beatha ameshukuru Halmashauri ya wilaya ya Karatu kwa kuwezesha kupata vifaa hivyo vinavyotumika katika shughuli zao za uuzaji wa maziwa. Lakini pia kwa kuendelea kuwapa mkopo ambao umewasaidia katika kupiga hatua zaidi katika shughuli zao za kuuza maziwa ya ng'ombe.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa