• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WA NGANO WAFURAHIA SERIKALI YA JPM

Posted on: January 29th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Mkataba` wa wakulima wa ngano na wakala wa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko kanda ya kaskazini uandikwe kwa Kiswahili ili kila mtu asome na kuuelewa. Kabla ya kusainiwa kwa mkataba ni lazima upitiwe na mwanasheria wa Halmashauri  akiwa na wajumbe wa pande zote mbili wa chama cha ushirika na bodi ili kujiridhisha kama mkataba unatija kwa pande zote.

Mh. Abbas Kayanda amesema hayo wakati alipofanya mkutano na wakulima wa ngano wilayani Karatu katika Ukumbi wa Halmashauri. Amesema maafisa ugani lazima watoke ofisini na wagawane maeneo ya kwenda kusaidia wakulima namna bora ya kufanya kilimo cha kisasa, ikiwa ni pamoja kuanzisha mashamba darasa ya ngano na  kufanya ufuatiliaji kwa wakulima  mara kwa mara.

Mh. Kayanda ameelekeza Maafisa ushirika kufufua vyama vya ushirika kwenye maeneo ambayo vyama vya ushirika vimekufa. Amesema lazima vyama vya ushirika vianzishwe na viweze kuimarishwa ili wakulima waweze kunufaika kwa kupata mkopo. Ameomba wakulima kuzingatia maelekezo waliyopewa na wataalamu ili waweze kujikita katika uzalishaji wa kilimo cha ngano chenye tija na kuepukana na ubadhilifu. Amesema wakulima watakofanya udanganyifu hatua  za kisheria zitachukuliwa dhidi yao kwa sababu watakuwa wanaharibu sifa nzuri tulionayo wakulima wa Karatu kwenye kilimo cha ngano.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda ( wa kwanza kushoto) akizungumza na wakulima wa ngano 

Mh. Kayanda ameomba wananchi kuacha kuchakachua mbegu za ngano jambo ambalo linasababisha kushindwa kupata ngano inayokubalika na wenye makampuni. Amesema hii ni fursa kwa wakulima kuongeza kiasi cha ngano ianayozalishwa nchini kwasababu soko la uhakika limepatikana. Amesema serikali kupitia wizara ya kilimo imedhamiria kufufua kilimo cha ngano, sasa bei ya kilo moja ya ngano itanunuliwa kwa Tsh. 800 kutoka Tsh 650.

Meneja wa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko kanda ya kaskazini ndg. Hiza Kiluwasha amesema lazima wakulima kufanya kilimo chenye tija na kwa kupanda mbegu bora na kufuta maelezo ya maafisa ugani. Amesema mkulima akipanda mbegu bora za ngano na mkulima kwa kufuata maelekezo ya wataalamu, ya kuandaa shamba, kutumia mbolea sahihi, na dawa sahihi kwa wakati muafaka mkulima anauwezo wa kupata gunia 12 kwa hekari na kuendelea. Hivyo wakulima wadogo na wakulima wakubwa ni vyema kujiunga na vyama vya ushirika. Vyama vya ushirika vilivyo hakikiwa na mrajisi ndivyo vitakavyoingia mkataba na bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko kwa ajili ya kusambaziwa mbegu.

Ndg. Kiluwasha  amesema utaratibu utakaotumika sasa mbegu za ngano zitasambazwa kupitia vyama vya ushirika kwa wakulima wadogo isipokuwa kwa wakulima wakubwa kuanzia hekari 50 ambao watachukuliwa mmoja mmoja. Mkataba ambao chama cha ushirika  itakaoingia na wakala wa bodi ya nafaka ndio utasaidia vyama vya ushirika kununua  ngano. Amesema vyama vya ushirika ndivyo vitakavyolipwa na kuja kulipa wakulima. 

 picha za matukio tofauti wakati wa kikao cha wakulima wa ngano na Mh. Abbas Kayanda

Meneja wa shirika la bima ya taifa mazao Mkoa wa Arusha ndg. John Mdenye amesema kuna bima ya mkopo atakaopata mkulima. Amesema huwa bima hiyo inasaidia kumlipa mkulima mkopaji pindi anapopata tatizo litakalomfanya asiweze kulipa mkopo. Amesema wameweka bima hyo kwa sababu kuna sababu mbalimbali  kama kuugua kifo zinazomfanya  mkulima aliyekata bima ya mkopo kushindwa kulipa.

Amesema kuna bima ya mazao kwa mkulima kwa mambo ambayo yapo nje ya uwezo wa mkulima, amesema bima hii inamasaidia kwenye changamoto ya ukame  mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababisha mafuriko, upepo unaoharibu mazao, magonjwa ya mazao au wadudu ambao hawana dawa. Mkulima anapaswa kuleta mapatao yanayopatikana kutokana mauzo ya mazao kwenye shamba lake lakini pia gharama za uazalishaji.

Mkulima wa ngano ndg. John Tippe ameshukuru serikali kwa mapango wa kuboresha kilimo cha ngano. Amesema serikali itengeneze mbegu za kutosha za ngano ili kupunguza gharama za kuchukua mbegu kutoka nje ya nchi. Amesema kuchukua mbegu nje ya nchi ni kunufaisha nchi nyingine, amesema sasa serikali ifikirie namna ya kuwapa mikopo wakulima wadogo wadogo ili waweze  kuwa na zana za kisasa za kilimo.


Matukio tofauti tofauti katika picha wakati wa kikao

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa