• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAKUU WA WILAYA KUPOKEA TAARIFA ZA MWEZI ZA MIRADI

Posted on: October 19th, 2018

Mkuu wa  mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo jana amefanya ziara Wilayani Karatu. Katika kikao cha ndani kilichofanyika Ukumbi wa Mkuu wa Wilaya, alizungumza na watendaji mbalimbali wa Wilaya ya Karatu.

Mheshimiwa Mrisho Gambo amewaelekeza Wakuu wa Wilaya katika Mkoa wa Arusha, kupokea taarifa za miradi ya kila mwezi ili kuweza kujua mapungufu na changamoto zinazokabili miradi hiyo ili kuchukua hatua stahiki na miradi hiyo iweze kwenda haraka.

Mheshimiwa Mrisho Gambo  amesema hajaridhishwa na makandarasi wa Maji Makina, ambaye alipewa miradi wa maji lakini miradi hiyo imeshindwa kufikia kiwango. Amesema Mkandarasi Makina alipewa mradi wa maji Kansay ambao alilipwa Million 444 kati ya million 467, lakini mkataba ulivunjwa baada ya kushindwa  kufikia viwango vya ubora. Mkandarasi huyo akapewa mradi wa maji Burger ambao nao alilipwa million 359 kati ya million 413, mkataba  ukavunjwa kwa sababu alishindwa kufikia viwango. Mkandarasi huyo akapewa mradi wa maji Matala akalipwa million 316 kati ya Million 375 mkataba ukavunjwa. Mheshimiwa Mrisho Gambo akamuelekeza Mkuu wa Wilaya Kuchukua hatua kali dhidi ya Mkandarasi huyo.

Mheshimiwa Mrisho Gambo alipokea taarifa ya mradi wa umeme vijijini REA phase three round one, Meneja wa Tanesco Karatu Ndugu Edward Mwakapuja alisema vijiji 9 vilikuwa kwenye mpango ambavyo vinajumuisha vitongoji 39. Alisema mpaka sasa Mhandisi amefanya kazi katika vijiji viwili tu ambavyo ni Kilimamoja na Kinihhe. Matarajio yetu mpaka sasa, kwenye mradi huu ni kwamba Mkandarasi angekuwa amefanya nusu ya kazi 50% lakini mpaka sasa Mkandarasi yupo chini ya 20%. Licha ya kuandikiwa barua ya onyo kutokana na utekelezaji mdogo wa mradi.

Mhandisi wa mradi huo NIPO GROUP L.T.D Engineer, Hussein Saidi alisema wanakutana na changamoto ya usambazaji duni kwa Wakala wa Usambazaji anayewaletea nguzo za umeme.  Aliongeza kusema mahitaji ya nguzo kubwa za umeme ni  nguzo 730 lakini wananguzo 257. Alisema mahitaji ya nguzo ndogo ni nguzo 1661 lakini nguzo walizo nazo ni 295. Engineer Hussein alisema wanauhitaji wa transfoma za umeme 50 lakini mpaka sasa wanatransfoma 21.

Mheshimiwa Mrisho Gambo amesema wananchi wanamatarajio makubwa ya kupata umeme katika makazi yao. Amesema sisi kama watendaji tunaomuwakilisha Mheshimiwa Rais lazima tutimize adhima ya kila sehemu kupata umeme ifikapo Mwaka 2021. Mheshimiwa Mrisho Gambo amewaonya watendaji wasio waadilifu wa Tanesco wanaowatoza wananchi zaidi ya kiwango kilichowekwa cha elfu 27000 ili kumuunganishia mwananchi na huduma ya umeme.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa