• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WALIMU KUJIELEZA KWA BARUA SHULE ZILIZOFANYA VIBAYA

Posted on: July 27th, 2019

Afisa elimu sekondari Bi, Kalista Maina ameendelea na ziara yake ya kutembelea shule za sekondari wilayani karatu. Ziara yake imelenga kujionea utendaji kazi wa walimu pamoja na kutambua kero za kitaaluma katika maeneo yao ya utendaji kazi.

katika ziara yake shule ya sekondari Florian amesema shule hiyo imezidi kushuka kitaaluma ukilinganisha na matokeo ya awali ya mtihani wa moko waliofanya. Shule hiyo ni shule ya 27 kati ya shule 32 za wilaya. Shule ya sekondari Florian haina ufaulu wa daraja la kwanza wala daraja la pili, ufaulu umeanza daraja la tatu. Matokeo haya kuanzia shule ya sekondari ya Welwel ambayo imekuwa ya 20 mpaka shule ya 32, waalimu wanaofundisha kidato cha nne katika shule hizo waandike barua kwa mwajiri kujieleza wamejipanga kwa namna gani kuinua ufaulu. Walimu 3 waliopata  daraja “F” ambao ni mwalimu wa bailojia, fizikia, na hesabu wataitwa kujieleza kwa muajiri, knamna watakavyo ondoa "F" na kuongeza ufaulu matokeo ya kidato cha nne. 

Bi, Maina amesema shule ya sekondari Florian ni shule kubwa, haiendani na hadhi ya ufaulu duni uliojitokeza kwa mtihani wa moko kidato cha nne. Ametoa maagizo kwa walimu wa shule hiyo kujipanga kwa kipindi cha miezi mitatu ili kupata matokeo mazuri kwenye mtihani wa taifa. Amewakumbusha muundo wa mtihani wa taifa ulivyobadilika na ametoa maelekezo kwa walimu kuwapa wanafunzi mazoezi ya mitihani kulingana na muundo huo wa mtihani.

Bi, Maina amesema kuwapa wanafunzi mazoezi ya maswali kunamsaidia mwalimu hata namna ya kufundisha kwa sababu kuna wakati mitaala yetu ilibadilishwa na kuletwa nyingine. Bado kuna mambo ambayo hayapo kwenye mitaala mpya ila yanatoka kwenye mtihani kwa mfumo wa mitaala ya zamani. Bi, Maina amesema mazoezi mengi maswali yanasaidia mwalimu kuandaa vyema andalio la somo kulingana na mahitaji. Ameongeza kusema maneno mahususi yanayotumika kwenye mtihani yanamsaidia mwalimu kuandaa maudhui yanayoendana na somo husika.   

Afisa elimu taaluma ndugu Robert Sijaona amesema kwa ukaguzi walioufanya wameona kuna ukwepaji wa kufundisha masomo kwa kiasi kikubwa sana. Amesema kwa kidato cha kwanza mkondo “A” pekee kuna vipindi 159 vya masomo tofauti tofauti ambavyo havijafundishwa. Sasa ni wakati wa kubadilika kiutendaji, walimu hatuzingatii misingi ya taaluma yetu. Kuna ujazaji shajara ambao haufuati utaratibu, amesema shajara zilizojazawa nyingi hazijawekwa saini na mkuu wa shuke wala mwalimu wa taaluma. Amesema hii inaonesha wadhibiti ubora wa ndani ya shule hawatekelezi majukumu yao vizuri jambo linalodumaza maendeleo ya taaluma.  Shule imeanguka kwa nafasi 50 kwenda chini, mwaka jana ilishika nafasi ya 155 katika matokeo ya moko na mwaka huu imeshika nafasi ya 206 kati ya shule 226. Tufanye kazi zetu vizuri na tuzingatie taratibu, vitu vilivyowekwa ni msingi wa ufundishaji ambao unaleta matokeo chanya kwa wanafunzi.  Amesema shule kongwe yenye kidato cha tano na sita haipaswi kuwa na ufaulu duni kiasi hicho.

Ndugu Robert Sijaona amesema lazima walimu tufundishe kwa malengo na hatuwezi kufundisha kwa malengo bila kufuata utaratibu. amesema kwenye kuandaa andalio la somo kuna vitu vinabadilika kila siku, lazima sasa walimu waliopata semina Karatu sekondari juu ya namna ya kuandaa andalio watoe elimu hiyo kwa wenzao. Ametoa maalekezo kwa walimu waliopata semina kuaanda andalio la kazi, kutenga siku kwa ajili ya kuelekeza walimu wenzao.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa