• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAZAZI WENYE WANAFUNZI WATORO KUPAMBANA NA MKONO WA SHERIA MATALA

Posted on: August 13th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Mkuu wa wilaya ya karatu Mh. Abbas Kayanda ameelekeza kukakamatwa kwa wanafunzi watatu, wanaosoma shule ya Msingi Matala na Njoro. Wanafunzi hao inadaiwa wamekataa kuendelea na shughuli za kimasomo ikidaiwa wanataka kuolewa.

Hayo yamesemwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Matala, malekezo hayo yametolewa baada ya wanafunzi hao kupata udhamini wa kusomeshwa na MO-Dweji.  Mh. Kayanda amesema pamoja na wanafunzi hao kukamatwa ameelekeza kukamatwa kwa watu ambao  wameshawishi mabinti hao, kutaka kuolewa. Amesema wazazi wa watoto hao wanaozuiwa watoto hao kusoma nao pia wakamatwe kwa sababu kumzuia mtoto wa shule kusoma ni dhuluma. Ameelekeza wazazi wanaohusika na watoto hao, baada ya kukamatwa kufikishwa mahakamani ili sheria zichukuliwe dhidi yao.

Mkuu wa wilaya ya Karatu, Mh. Abbas Kayanda akizungumza na wananchi wa Matala.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karatu Ndg. Waziri Mourice amesema katika shule ya Msingi Njoro na Matala kuna ufadhili wa Mohamedi Dweji kwa wanafunzi watatu ili kuwasaidia kuweza kusoma. Amesema baada ya kipindi cha mapuziko cha corona wanafunzi hao hawakurudi shuleni mpaka sasa. Amesema mmoja katika wale wawili wa Matala anafanyiwa mpango wa kuozeshwa. Ndg. Mourice amesema wazazi hao wamefanya makusudi kutowarudisha wanafunzi hao shuleni.

Sambamba  na hilo Ndg. Mourice amesema ataleta mwalimu wa kike shule ya msingi Matala na watapeleka walimu wa kike shule ya msingi Njoro. Amesema wanafunzi wa kike wamekuwa wakipata shida sana hasa kupata mwalimu anayeweza kuwasikiliza na kuwalea wanafunzi wa kike.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu Ndg. Waziri Mourice akieleza hali ya utoro wa wanafunzi katika Kijiji cha Matala. 

Naye Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Matala  Iddi Kiboko amesema changamoto kubwa wanayopata kwa wanafunzi wa Matala ni kutokuwa na mahudhurio mazuri darasani. Amesema wakati wanafunzi wanaposhindwa kuhudhuria darasani kwa siku tano zinazopangwa  kwa juma zinafanya mwanafunzi kukosa baadhi ya vitu vinavyofundishwa darasani. Amesema hali hiyo ndiyo inayosababisha baadhi ya wanafunzi kufika darasa la saba bila kujua kusoma na kuandika.

Amesema ili kusadia hali hiyo wazazi wanapaswa kuwasimamia wanafunzi wao kwa kuhakikisha wanakuwa wanamahudhurio mazuri shuleni. Mwalimu Kiboko amesema lazima wazazi pia wafuatilie maendeleo ya wanafunzi wao shuleni kwa kuhakikisha kazi za darasani wanazopewa zinafanyika, amesema ushirikiano wa mzazi na mwalimu ndio utakaosaidia kuinua kiwango cha ufaulu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa