• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI TISINI NA TISA WAATHIRIKA NA MVUA MANG’OLA

Posted on: February 4th, 2020

Mkuu wa wilaya ya karatu Mhe. Theresia Mahongo, ametembelea na kuzungumza na waathirika wa mafuriko yaliyotokea kata ya Mang’ola. Katika ziara hiyo mkuu wa wilaya aliambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya.

Mhe. Mahongo ametembelea kijiji cha Langharerir ambacho waanachi 15 nyumba zao zimebomolewa na mvua zinazoendelea kunyesha. Malechand wananchi 30 nyumba zao zimeathirika na mafuriko ya maji ya mvua na Mang’ola barazani nyumba 44 zimebomoka kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha. Mhe. Mahongo amewapa pole na ametoa wito kwa wananchi waliojenga na wanaoendelea kujenga nyumba katika mikondo ya maji kuondoka maeneo hayo, kwa sababu si maeneo salama. Amesisitiza wananchi kujenga nyumba za kudumu katika maeneo ambayo hakuna mikondo ya maji. Mhe. Mahongo amewataadharisha wananchi kwamba katika siku tano mfululizo mvua kubwa zinatarajiwa kunyesha amesema ni vyema watu wanao ishi mabondeni na kwenye mikondo ya maji kuchukua tahadhari na kuondoka maeneo hayo.

Mhe. Theresia Mahongo akimuhimiza mama Tumaini aliye Kushoto huko kijiji cha Langharer kuhama nyumba hiyo, iliyoharibika vibaya kama inavyoonekana nyuma ya picha.


Mhe. Mahongo amesema Malechand kuna drif ambalo limejengwa kwa mwinuko badala kuwa kwa mteremko ndio iliyochangia maji kufurika na kuingia kwenye makazi ya watu. Amesema drift hiyo itatabomolewa na utajengwa mfereji, amewapongeza wananchi wa Malechand kwa kuchukua tahadhari mapema. kuondoka maeneo yenye mafuriko na kutafuta makazi ya muda, Mhe. Mahongo amesema kwa sababu waathirika wameshatoka amelekeza uongozi wa Malechand kukaa kikao cha kijiji ili kuweka utaratibu wa waathirika kuweka makazi ya muda katika ofisi za maji.

Mhe Mahongo amesema pamoja na wananchi hao kukaaa katika eneo hilo la muda ametoa maelekezo ya viongozi wa kijiji kuweka katika maandishi mkataba na kuwapa waathirika hao ili waweze kukaa na kwa muda katika eneo hilo lilotengwa kwa makazi ya dharura. Lengo la kuandikisha ni kuepuka mkanganyiko siku za usoni juu ya namna walivyopewa idhini ya kuweka makazi ya Muda katika ofisi za maji zilizopo Malechand.

Mwenyekiti wa kijiji Malechand Marco Yoyo amesema kitendo cha kuwasiliana na wananchi wenzao walio nje ya Malechand kimewasaidia kuwapa taarifa mapema hivyo kunusuru athari za mafuriko. Ndugu Yoyo amesema kwa kushirikiana na Afisa tarafa walipiga la mbiu kuwapa tahadhari juu ya mafuriko. Amesema watu wasio na makazi walienda kujisitiri kwa ndugu jamaa na marafiki amesema hakuna mifugo iliyokwenda na maji.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa